Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU. |
Bwana YESU
atukuzwe ndugu yangu, karibu tujifunze Neno la MUNGU.
Ualimu wa
Neno la MUNGU ni moja ya huduma tano ambazo MUNGU amezitoa katika Kanisa lake.
Ili
kuukamilisha Mwili wa KRISTO ambao ni
Kanisa kunahitaji Mitume, Manabii, Wainjilisti, Wachungaji na Walimu.
Waefeso
4:11-12 ‘’ Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; ‘’
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; ‘’
Kila mwenye
wito wa huduma anatakiwa kutimiza majukumu yake.
Mimi binafsi
kama Peter Sitasahau mwaka mmoja Tarehe 2 Mwezi wa Nne ambapo ROHO MTAKATIFU alisema na mimi kwamba
ameniita katika Kazi ya ualimu wa Neno la MUNGU. Tangu siku hiyo nilijitambua
na kujielewa.
Kibinadamu kama ningeambiwa kuchagua huduma ya kumtumikia
Bwana YESU basi hakika ingekuwa vigumu kwangu kuchagua huduma ya ualimu. Lakini
hakuna Mkristo hata mmoja ambaye anaweza kujichagulia huduma ya kumtumikia
Bwana YESU.
ROHO
MTAKATIFU ndiye anayechagua watu kwa upendo wake mwenyewe.
Zamani
nilikuwa naomba juu ya karama ambazo nilitaka nimtumikie MUNGU kwa hizo lakini
nikakatazwa maana huwezi wewe mwanadamu kujichagulia huduma au karama utakayo
bali ROHO MTAKATIFU ndiye hugawa kama
vile apendavyo yeye.
Katika
Kanisa la leo huduma zimekuwa kama vyeo, Hayo ni makosa makubwa.
Kuna watu
leo ingawa wamepewa kuwa Walimu au
wainjilisti, wao wameamua kujiita Mitume au Manabii wakidhani kuwa Mtume au
Nabii ni kupata heshima kubwa, wengine wamejiita Mitume au Manabii ili
kujitafutia mali ndio maana Katika Kanisa leo Walimu ni Wachache sana.
Jambo muhimu
sana kwa kila mtu aliyeitwa katika
huduma fulani katika Mwili wa KRISTO anatakiwa abaki katika huduma yake.
Katika
Kanisa majina ya huduma hayana maana
sana kama mhusika haifanyi kazi yake aliyoitiwa.
Kama
utajiita Mchungaji harafu huna kondoo hata mmoja uliyemshuhudia basi wewe sio
Mchungaji.
Kama
utajiita Nabii wakati hufanyi kazi za Nabii hakika wewe sio Nabii.
Kama
utajiita Mtume na hujawahi kufungua hata makanisa 50 basi wewe sio Mtume.
Kama
utajiita Mwinjilisti na hujawahi kuwaleta kwa YESU hata watu 20 basi wewe sio
Mwinjilisti.
Kumbuka
MUNGU alituita kwa kusudi na yeye ndiye hufanya kazi zake kupitia sisi, hivyo
ukikataa wito au kujichagulia wito utajikuta unafanya kazi peke yako maana umelikataa shauri la MUNGU.
Wafilipi
2:13 ‘’Kwa maana ndiye MUNGU atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
‘’
Leo
nazungumzia kazi za Mwalimu wa Neno la MUNGU.
Kazi za
Mwalimu wa Neno la MUNGU.
1. Kuwafanya
watu kuwa wanafunzi wa YESU.
Mathayo 28:19 ‘’ Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;‘’
Mathayo 28:19 ‘’ Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;‘’
Kazi ya kwanza kabisa ya kila mwalimu wa Neno la MUNGU ni kuwafanya watu
wote anaowafundisha kuwa wanafunzi wa YESU.
Mwalimu wa Neno la MUNGU anatakiwa kuzingatia hilo siku zote za utumishi
wake katika kazi ya MUNGU.
Ni YESU KRISTO Mwenyewe alisema kwamba tuende Duniani kote ili tu
tukawafanye watu wote kuwa wanafunzi wake.
Wanafunzi wa YESU ni wale ambao wako tayari kujifunza kwa YESU huku
wakiwa wamempokea yeye kama Mwokozi wao.
Usikubali kuwa Mwalimu wa Neno la MUNGU wa kuwafundisha watu kuwa
wanafunzi wako, bali wafanye wawe wanafunzi wa YESU.
Usikubali kuwa Mwalimu wa Neno la MUNGU wa kuwafanya watu wawe wanafunzi
wa dhehebu lako, bali wafanye kuwa wanafunzi wa YESU wanaomtii MUNGU katika
YESU KRISTO.
Usikubali kuwa mwalimu wa Neno la MUNGU wa kuwafanya watu kuwa wanafunzi
wa mwanzilishi wa dhehebu lako aliye mwanadamu, bali wafanye watu wote kuwa
wanafunzi wa YESU KRISTO.
Kumbuka hakuna Mwokozi nje na YESU KRISTO Yohana 14:6 na kumbuka pia
Bwana YESU alikuwa kuwatafuta watu wote
ili wawe wanafunzi wake
Hivyo epuka sana kuwafanya watu kuwa wanafunzi wako bali wafundishe jinsi
ya kuwa wanafunzi wa YESU KRISTO.
Ukizingatia hayo huku ukifanya huduma yako kwa bidii hakika utakuwa
Mwalimu mzuri wa Neno la MUNGU.
2. Kuwafundisha
watu kuyashika yote aliyofundisha Bwana YESU.
Mathayo 28:20 ‘’ na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.‘’
Mathayo 28:20 ‘’ na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.‘’
Hii ni kazi muhimu sana kuizingatia kila mwalimu wa Neno la MUNGU.
Hakikisha unawafundisha watu kuyashika yote aliyofundisha Bwana YESU.
Bwana YESU alifundisha kwa miaka 3
mambo mengi sana na hayo kama msingi yako katika injili zake nne.
Ukisoma agano jipya lote linarudia tu kile alichofundisha Bwana YESU.
Agano la kale pia lina ufunuo mkubwa mno kuhusu YESU KRISTO na mafundisho
yake.
Mafundisho makuu ya YESU ni injili yake ya wokovu wa milele.
Kwa hiyo hata unapolisoma agano la kale lisome na kwa jinsi ya KRISTO na
fundisha watu kwa jinsi ya KRISTO maana huu ndio wakati wa injili iokoayo na wakati
huu utaenda hadi kurudi kwa YESU.
Hakuna kitu ambacho YESU alibakiza katika mafundisho yake hivyo
alipokamilisha kazi aliagiza wafundishaji wote wa Neno la MUNGU kufundisha watu
wote kuyashika aliyofundisha.
Tunapofundisha kuyashika
aliyoyafundisha Bwana YESU hatuna maana ya kwamba tufundishe watu kusoma
Vitabu vinne tu vya Mwanzo vya agano
jipya ambavyo ndivyo vinafunua injili yake, bali tusome Biblia nzima huku tukijua kwamba huu ni
wakati wa injili ya KRISTO, Ukijua hivyo utakuwa mwalimu mzuri wa Neno la MUNGU
usiyewachanganya watu.
Tunajua kabisa kulikuwa na wakati wa Watu kuongozwa Dhamiri zao wenyewe,
leo hatuwezi kuwafundisha watu kuongozwa
na dhamiri zao wenyewe, bali leo tunawafundisha watu kuongozwa na ROHO
MTAKATIFU.
Tunajaua kuna wakati ulikuwa wakati wa torati, leo hatuwezi kuwafundisha
watu kushika torati wakati tuko na KRISTO na
sio torati.
Wakati huu ni wa injili hivyo ni lazima tuhubiri injili ili watu
waokolewe na KRISTO na ili watu wafunguliwe
na KRISTO.
Ukiniuliza kazi mbili zilizomfanya YESU kuja duniani nitajikujibu hivi.
a.
YESU
alikuja kutafuta na kuokoa watu wote maana wote tulikuwa tumepotea.
Luka 19:10 '' Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.''
b.
YESU
alikuja kuziharibu kazi zote za shetani.
1 Yohana 3:8 ‘’ Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. ‘’
Hivyo ni lazima
tuwafundishe watu kuyashika yote
aliyofundisha YESU huku tukiwaombea ili YESU awafungue vifungo.
YESU anataka kumweka huru
kila mtu
Yohana 8:36 ''Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.
''
Hivyo ni lazima sana
tuwafundishe watu kuyashika yote aliyofundisha YESU. YESU alifundisha watu wote
kumpokea kama Mwokozi, usipompokea YESU kama Mwokozi umepotea.
YESU alifundisha
kumwabudu MUNGU katika roho na kweli.
YESU alifundisha
utakatifu n.k
Hayo ndiyo ambayo YESU
anatuagiza walimu wote wa Neno la MUNGU kuwafundisha watu wote kuyashika.
3.
Kujibu
kibiblia maswali yote yanayowatatiza watu kuhusu Wokovu wengine .
1 Petro 3:15 ''Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. ''
1 Petro 3:15 ''Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu. ''
Hii ni kazi muhimu sana
ya mwalimu wa Neno la MUNGU yaani kujibu maswali kuhusu tumaini lako la wokovu.
Katika Elimu ya Kidunia
Mwalimu hujibu maswali ya wanafunzi wake ili wanafunzi waelewe kwa usahihi,
hata wewe mwalimu wa Neno la MUNGU inakupasa kuwa mtu wa kujibu maswali ya
wanafunzi wako maana umeitwa katika ualimu basi ulijue na hilo.
Ili uweze kujibu vyema
maswali ya wanafunzi wako ni lazima sana wewe mwenyewe uwe mtu wa kujifunza
sana sana.
Haiwezekana Mwalimu
unafundisha kila siku watu kuokoka kisha mwanafunzi akuuulize kwamba kuokoka ni
nini kisha wewe useme sijui, hakika wewe utakuwa sio Mwalimu sahihi wa Neno la
MUNGU. Mtu akuulize Wokovu ni nini, wewe useme hujui wakati umefundisha kwa
msisitizo mkubwa kuhusu wokovu, ndugu ukijijua wewe ni mwalimu wa Neno la MUNGU
hakikisha unajifunza sana Neno la MUNGU na hata kujifunza kwa watumishi wa
KRISTO wengine ili uelewe kwa upana zaidi.
Hakikisha unajua kabisa
kwamba kujibu Maswali kuhusu MUNGU, kuhusu YESU, kuhusu ROHO MTAKATIFU, kuhusu
Kanisa, Kuhusu Injili na kuhusu Biblia nzima hakikisha unajua ili upate
kuwasaidia watu wengi.
Pia katika kila somo
unalofundisha hakikisha ukiulizwa swali kutokea katika somo hilo hakikisha
unajibu, maana huwezi kufundisha kitu usichokijua.
Najua kabisa kuna wakati ukifundisha mfano ibada kuu Kanisani
hakuna maswali kuulizwa lakini katika madarasa huru mfano Sunday School
ukiulizwa swali lijibu na hata kama umefundisha mfano kwenye mkutano wa injili au ibada kuu na hakukuwa na nafasi ya
kuulizwa maswali basi ikitokea mtu baada ya ibada akataka umweleweshe kulingana
na somo lako basi mjibu vyema maana ni moja ya kazi zako kujibu maswali ya watu
wa MUNGU kuhusu MUNGU wao na mpango wake kwao.
Kuna watumishi akiulizwa
swali tu basi anachukia na anawaona
waulizaji kuwa ni watu wakorofi tu, kumbe kuna wengine kabisa wanataka tu
kuelewe ili wafanyie kazi kwa usahihi.
(unaweza ku-search pia Somo langu linalotiwa aina za
maswali na utajifunza aina mbalimbali za maswali na jinsi ya kujibu)
4.
Kuwafundisha
watu kutafakari Neno la MUNGU.
Zaburi 27:4 ‘’ Neno Moja nimelitaka kwa BWANA, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa BWANA Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa BWANA, Na kutafakari hekaluni mwake. ‘’
Zaburi 27:4 ‘’ Neno Moja nimelitaka kwa BWANA, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa BWANA Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa BWANA, Na kutafakari hekaluni mwake. ‘’
5.
Kuwafanya
watu wa MUNGU wasikate tamaa katika maisha ya safari ya wokovu.
Luka 18:1 ‘’ Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba MUNGU sikuzote, wala wasikate tamaa.‘’
Luka 18:1 ‘’ Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba MUNGU sikuzote, wala wasikate tamaa.‘’
6.
Kuisikiliza
sana sauti ya ROHO MTAKATIFU na kuifanyia kazi katika mwili wa KRISTO.
Kumbu 28:1 ‘’ Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; ‘’
Kumbu 28:1 ‘’ Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; ‘’
7.
Kujifunza
sana kwa KRISTO ili upate kitu cha kuwafundisha watu.
Mathayo 11:29a ''Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; ''
Mathayo 11:29a ''Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; ''
8.
Kuweka Misingi mizuri ya Kiroho kwa
unaowafundisha.
Misingi ya kiroho ipo mingi sana baadhi ya misingi muhimu
ambayo unatakiwa wewe mwalimu wa Neno la MUNGU kuiweka katika Kanisa ni hii.
Misingi muhimu zaidi ni pamoja na hii.
1.
Utakatifu.
1 Petro 1:15 ''bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;''
2. Wokovu wa KRISTO .
Yohana 14:6 '' YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba(MUNGU), ila kwa njia ya mimi. '' Pia soma Matendo 4:12 na Luka 19:10
1 Petro 1:15 ''bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;''
2. Wokovu wa KRISTO .
Yohana 14:6 '' YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba(MUNGU), ila kwa njia ya mimi. '' Pia soma Matendo 4:12 na Luka 19:10
3.
Imani
.
Warumi 10:17 ''Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la KRISTO. '',
Pia soma Waebrania 11:6
Warumi 10:17 ''Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la KRISTO. '',
Pia soma Waebrania 11:6
4.
Utoaji.
2 Kor 9:6-7 '' Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana MUNGU humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. ''
2 Kor 9:6-7 '' Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana MUNGU humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. ''
5.
Kumtegemea
MUNGU.
Yeremia 17:7 ''Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.''
Yeremia 17:7 ''Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.''
6.
Maombi.
1 Thesalonike 5:17 '' ombeni bila kukoma; ''
1 Thesalonike 5:17 '' ombeni bila kukoma; ''
7.
ROHO
MTAKATIFU na nguvu zake .
Yohana 14:16-17 ''Nami nitamwomba Baba(MUNGU), naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye ROHO wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. '',
Pia soma Matendo 1:8, Wagalatia 5:25, Warumi 8:14
Yohana 14:16-17 ''Nami nitamwomba Baba(MUNGU), naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye ROHO wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. '',
Pia soma Matendo 1:8, Wagalatia 5:25, Warumi 8:14
8.
Kukataa
dhambi zote na kujitenga mbali nazo.
Zaburi 34:14 '' Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie. ''
Zaburi 34:14 '' Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie. ''
9.
Toba.
Matendo 3:19 ''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA; ''
Mathayo 3:2, Isaya 55:6-7
Matendo 3:19 ''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA; ''
Mathayo 3:2, Isaya 55:6-7
10.
Kushuhudia
injili na kuikiri hadharani.
Marko 16:15-16 ''Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. ''
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292(Hadi whatsapp).
+255786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Marko 16:15-16 ''Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. ''
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292(Hadi whatsapp).
+255786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Comments