MTESI NI NANI.

 

Na Mwl Peter Mabula



Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu zangu wote. 

Rafiki yangu mmoja aliniuliza swali hili, aliniandikia hivi "Mchungaji Peter Mabula naomba kuuliza.

 Huwa nikisoma maneno ya MUNGU  nakutana na neno "Watesi/Mtesi"  silijui maana yake naomba unifafanulie pamoja na neno kutiisha."


Mimi Peter Nachukua nafasi kujibu kuhusu Watesi /Mtesi na siku nyingine nitajibu kuhusu "Kutiisha"


Majibu yangu ni haya.  


 Neno  "Mtesi" lina maana hizi mbili. 


1. Mtesi ni mtu mwenye tabia ya kugombana. 


Hivyo Mtesi wako ni mtu yule mwenye tabia ya kugombana na wewe kila muda katika jambo lolote au mtu ni mwenye tabia ya kutaka kugombana na wewe katika mambo mbalimbali hata kama hujamkosea. 


2. Maana ya pili ya neno "Mtesi" Ni mtu pia mwenye mazoea ya kusengenya.


Hivyo Kibiblia mtu ambaye ana tabia ya kukusengenya huyo ndio Mtesi wako.


Unaweza ukajikuta una  Mtesi iwe ni kazini au nyumbani au mitaani kwenu au kwenye ukoo n.k  


Watesi wakati mwingine wanaweza kukukatisha tamaa sana. 


Zaburi 3:-2 " BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, Ni wengi wanaonishambulia, Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, Hana wokovu huyu kwa MUNGU."


Nini ufanye kuhusu Mtesi anayekusumbua. 


1.  Omba Bwana YESU KRISTO akupe kinywa na hekima ambavyo huyo Mtesi wako hatashindana navyo. 


Luka 21:15 "kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga."


2.  Omba MUNGU akuokoe dhidi ya Mtesi wako. 


Zaburi 44:7 "Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu; Na watuchukiao umewaaibisha."


3.  Kaa kwenye Kusudi la MUNGU la Wokovu wa KRISTO kwa utakatifu wote na MUNGU atakuinua juu ya huyo Mtesi wako. 


Zaburi 23:5-6 " Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele."


4.  Mtesi akizidi sana na wewe hujamkosea kwa lolote basi omba MUNGU amwadhibu. 

 

Zaburi 60:12 "Kwa msaada wa MUNGU tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu."

MUNGU akubariki sana. 

By Peter Mabula. 

Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi.

+255714252292


Ubarikiwe

Comments