Bwana YESU KRISTO Mwokozi wetu atukuzwe ndugu zangu wote.
Katika
safari yangu ya utumishi nimewahi kukutana na marafiki ambao walikuwa
vizuri sana na MUNGU na nguvu za MUNGU zilikuwa ndani Yao lakini baadae
nikaambiwa wameacha Wokovu nilisikitika sana na kuumia sana moyoni.
Nilichogundua kwao shetani ndani ya mioyo yao alikuwa amefuta kumbukumbu za Kukumbuka wema wa MUNGU.

Kumbu
4:9 "Lakini, jihadhari nafsi yako, ukailinde roho yako kwa bidii, usije
ukayasahau mambo yale uliyoyaona kwa macho yako, yakaondoka moyoni
mwako siku zote za maisha yako; bali uwajulishe watoto wako na watoto wa
watoto wako;"
Inawezekana bado hujanielewa, ngoja niseme kwa mifano hali iliyowahi kutokea.
Dada
mmoja ambaye tulikuwa tunaimba naye Kwaya Zanzibar na ambaye tulikuwa
tunafanya nae huduma ya kuombea watu Kanisani. Dada huyu baada ya kuona
amekaa muda mrefu kama miaka 2 bila kupata Mchumba akaamua kuacha
Wokovu.
Dada huyu alipokuwa ndani ya Wokovu
alikuwa na nguvu za MUNGU lakini alipoacha Wokovu nguvu za MUNGU
zikaondoka ndani yake akaanza kufuata wapinga KRISTO na waganga wa
kienyeji na kujikita amedanganyika. Baadae akajikuta amekuwa
mwasherati na amebebeshwa mimba maana hakuwa na hofu ya MUNGU tena. Siku
Moja akavamiwa na mapepo akaenda kwa mganga wa kienyeji na kufia huko,
inasikitisha sana
Ndugu zangu, wako watu wanalalamika kwamba MUNGU amewasahau na wanaacha Wokovu, ndugu nakuomba sana usiwe Wewe.
Watu
wengi MUNGU amewahi kuwasaidia na kuwaokoa kwa mengi sana lakini baadae
katika safari zao za maisha wanamwacha MUNGU. Hii ilitokea pia kwa
Waisraeli kipindi fulani.
Waamuzi
8:34 "Kwani wana wa Israeli hawakumkumbuka BWANA, Mungu wao, ambaye
ndiye aliyewaokoa na mikono ya adui zao wote pande zote;"


Kumbu 7:18 "Usiwaogope; kumbuka sana BWANA, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote;"
Kwanini Leo unalalamika MUNGU amekusahau wakati wakati yapo mambo mengi ambaye MUNGU amekutendea?
Ndugu kumbuka hata hayo ili umtukuze MUNGU na haya mahitaji ya Sasa atakutendea pia


Isaya
44:21 "Kumbuka haya, Ee Yakobo; nawe Israeli, maana wewe u mtumishi
wangu; nimekuumba; u mtumishi wangu; Ee Israeli, hutasahauliwa na mimi."
Wako watu Bwana YESU KRISTO aliwashindia dhidi ya wachawi, roho za mauti, mapepo, mizimu na miungu.



Napenda
kukuambia kwamba akina Hannah na Elizabeth walizaa wakiwa na umri
mkubwa kuliko Wewe na inawezekana walizaa wakiwa na umri mkubwa kuliko
hata umri wa Mama yako Mzazi.
Hebu ndugu mkumbuke MUNGU na Miujiza yake.
Ombea fahamu zako kama umefika hatua huoni wema wa MUNGU ingawa wema wa MUNGU upo.
Ndugu, unakumbuka YESU alikokutoa?
Kumbu 24:22 "Nawe kumbuka ya kuwa ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri; kwa hiyo nakuamuru kutenda neno hili."

Ulikuwa husameheki lakini kwa damu yake ya Agano jipya na kwa upendo wake akakusamehe, mbona unaanza kusahau wema wake.
Kuna watu Hadi Bwana YESU KRISTO awatazame kama alivyomtazama Petro ndipo watakumbuka.
Luka
22:61 "Bwana(YESU) akageuka akamtazama Petro. Petro akalikumbuka lile
neno la Bwana jinsi alivyomwambia, Leo kabla hajawika jogoo utanikana
mara tatu."
Nini ukumbuke?
1. Kumbuka njia aliyokuongoza MUNGU kwenye ushindi kabla
Kumbu
8:2 "Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza
miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua
yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo."
2. Kumbuka kabla ulikuwa kwa shetani kabla YESU KRISTO hajakuokoa na kukuandika jina lako kwenye Kitabu Cha Uzima Mbinguni
Kumbu
15:15 "Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri,
akakukomboa BWANA, Mungu wako; kwa hiyo mimi nakuamuru neno hili hivi
leo."
Nini ufanye katika Maombi
1. Katika Maombi ombea fahamu zako ili zikumbuke Matendo ya MUNGU.
Zaburi 77:11 "Nitayakumbuka matendo ya BWANA; Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale."
2.
Katika Maombi yako kataa hofu na ruhusu ufahamu wako kuona Yale Matendo
makuu ambayo MUNGU amewahi kuwatenda mawakala wa shetani hata
hawakukuonea.
Kumbu 7:18 "Usiwaogope; kumbuka sana BWANA, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote;"
3. Ombea fahamu zako zimkumbuke YESU KRISTO siku zote ili ubaki upande wake siku zote za maisha yako.
Zekaria
10:9 "Nami nitawapanda kama mbegu kati ya mataifa; nao watanikumbuka
katika nchi zilizo mbali; nao watakaa pamoja na watoto wao; tena
watarudi."
Omba ndugu yangu.
Omba katika jina la YESU KRISTO.
Ombea fahamu zako ili ziwe daima zinaona wema wa MUNGU.
MUNGU akubariki.
By Mwl Peter Mabula
+255714252292
Ubarikiwe
Comments