KAMA UNA AKILI ACHA UZINZI NA UASHERATI.

Na Mwl Peter Mabula, Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi 

 



Uzinzi na uasherati wakati huu umekuwa ndio sumaku kuu ya kuwanasa watu ili waende jehanamu.

Sumaki hii imewanasa hata ambao hawakutegemewa wala kutarajiwa.

Uzinzi uzinzi uzinzi umekuwa kama perfume ya kujipulizia kila Mara mtu akipenda.

Uasherati umekuwa kama heshima ya kibinadamu kwa vijana wengi.

Mbingu zimenyamaza kwa sababu iko jehanamu inawangoja wazinzi na waasherati wote.

1 Wakorintho 6:9 "Au hamjui ya kuwa wadhalimu HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU? Msidanganyike; WAASHERATI HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU, wala WAABUDU SANAMU, WALA WAZINZI, WALA WAFIRAJI, WALA WALAWITI,"

Dhambi hii imekuwa sumaku kubwa ya shetani ya kukamata wanadamu ili waende jehanamu.

Wanadamu walio wengi Leo ukimwambia kwamba aache uzinifu maana wazinzi na waasherati hawataenda uzima wa milele, mtu huyo anakuambia unamhukumu.

Ni Neno la MUNGU ndile limesema katika maandiko mengi tu kwamba wazinzi na waasherati sehemu yako itakuwa katika ziwa la moto.

Hata makanisani baadhi ya watu wamenasa kwenye sumaku hii.

Dada mmoja ambaye kila wiki anasimama na kushika mic Kanisani kwao siku moja aliniambia kwamba hawezi kumaliza wiki bila kufanya ngono, na hajaolewa. Niliumia sana rohoni nikamwambia aache kutumika madhabahuni, yeye akasema itakuaje maana yeye ndiye tegemeo.

Mama mmoja alisema yeye ana mume mwema sana na mume wake ni mwaminifu sana katika ndoa yao lakini yeye huyo mama ndio hutoka nje ya ndoa Mara kwa Mara, ni hatari inayohitaji neema ya MUNGU tu ili kutubu na kuacha.

Mama mmoja yeye ana watoto zaidi ya wawili na yuko katika ndoa lakini hana uhakika kama watoto wale ni wa mume wake wa ndoa, ni hatari sana.

Baba mmoja akiwa ndani ya ndoa amezaa watoto zaidi ya watatu nje ya ndoa tena wanawake zaidi ya wanne(4) tofauti tofauti.

Mwanaume moja ambaye husimama madhabahuni yeye kila Mara humdanganya mkewe kwamba anaenda safari kumbe ana mahawara karibia kila mkoa, ni hatari sana.

Watu wengi sasa wanaona uzinzi na uasherati ndio fashion nzuri ya wakati huu kwao.

Kila kijana ana girlfriend kwa lengo la ngono tu na sio vinginevyo.

Kila binti ana boyfriend kwa ajili ya uasherati.

Ukitaka watu wakuchukie basi kemea uzinzi na uasherati.

Watu wengi wamekuwa vipofu wa kiroho kwa sababu ya uzinzi na uasherati.

Lakini upo mwisho mmoja kwa watenda dhambi wote ambao ni jehanamu.

■Ndugu unahitaji kutubu Leo na kuacha dhambi.

1 Wathesalonike 4:1-4 " Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana YESU; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza MUNGU, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana YESU. Maana haya ndiyo mapenzi ya MUNGU, kutakaswa kwenu, MWEPUKANE NA UASHERATI; KILA MMOJA WENU AJUYE KUUWEZA MWILI WAKE KATIKA UTAKATIFU NA HESHIMA;"

Ndugu mmoja akasema yeye anaishi maisha matakatifu ila dhambi moja tu yaani uzinifu ndio imemshinda, hiyo ni hatari na ni ujinga uliopitiliza maana akizubaa anakosa mbingu.

Waefeso 5:3 "Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;"

Leo hata ndoa takatifu zimeadimika maana wahusika huanza kwanza uzinzi na uasherati ndio baadae ndoa, ndugu mnahitaji kutubu.

Ndugu yangu unayenisikiliza kwa njia ya ujumbe huu nakuomba tubu na acha dhambi hiyo, acha kwa faida ya roho yako.

Amua kuokoka kwa kumpokea YESU KRISTO kama hujaokoka.

Mwisho wa uzinzi na uasherati ni kifo(Mauti) na jehanamu.

Mwisho wa uzinzi na uasherati ni kifo(Mauti) na baada ya kifo ni hukumu(Waebrania 10:27)

Nimekuonya wewe Leo ili ukishupasa shingo usije ukalaumu siku ile ukiwa katikati ya bahari ya moto huku kifo kimezuiliwa ili uteseke milele.

Ni ROHO MTAKATIFU amenipa ujumbe huu live ili baadhi watubu na kumpokea Bwana YESU na kuokoka.

Mimi naamini utatengeneza ndugu baada ya kuusoma ujumbe huu.

Mimi naamini utaachana na mahawara na kuanza kuiheshimu ndoa yako.

Mimi naamini hutamsaliti tena mkeo/Mumeo.

Mimi naamini utaachana na huyo girlfriend/Boyfriend, wengine wanao zaidi ya mmoja, nakuomba ndugu achana nao wote.

Kijana au binti kaa tulia hadi wakati wako wa ndoa.

Mimi naamini utafunga safari kwenda Kanisa la kiroho kumweleze mchungaji ili akuongoze sala ya toba kisha utatubu na kuacha dhambi zote ikiwemo uzinzi au uasherati.

Uliyenisikia na utatubu na kuacha dhambi hiyo, MUNGU akubariki sana.
By Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi.

Naomba sambaza ujumbe huu kwa marafiki zako ambao hutaki waende jehanamu.

Comments