MWENYE SIKIO LA KUSIKIA ALIYE KANISANI ASIKIE LEO.

Mwl Peter Mabula, Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi 

 



Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu yangu.

Karibu nikujuze ufunuo huu nilioambiwa kwa ajili ya watu wa Kanisa.

■Nianze kwa kusema hivi Usipobadilika utaende jehanamu huku unaimba pambio, wewe mwimbaji ila mwasherati na mzinzi.

■Usipobadilika utaenda jehanamu na sauti yako yenye upako, wewe mhubiri ila mzinzi na mwasherati.

■Usipobadilika utaenda jehanamu huku nyimbo zako mwenyewe zikikusindikiza, kwa sababu tu wewe ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili ila mwasherati na mzinzi.

1 Wakorintho 6:9 " Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa MUNGU? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,"

■Uaskofu huku unaendelea na uzinzi wewe ni wa jehanamu, hata kama unaheshimika vipi hapa duniani.

■Uchungaji wa viwango lakini ni mzinzi, wewe ni wa jehanamu na sio mbinguni.

■Kuitwa Mtume au Nabii au Mwinjilisti au Mwalimu lakini huku wewe ukiendelea na uzinzi na uasherati wewe hakika ni wa jehanamu.

■Ukiwa mtoaji safi, mshirika sana na bado wewe ni mzinzi na mwasherati tambua kwamba YESU anasema

Mathayo 7:21-23 "Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu."

●Ndugu Mtumishi si unaendelea na uzinzi au usherati?

Ni rahisi sana kwamba YESU KRISTO atakuambia siku ukifa kwamba "Sikukujua wewe kamwe; ondoka kwangu, wewe mtendao maovu"

●Wewe uliyetumwa na shetani ili utembee na watu wa Kanisa wenzako ili wewe na wao mkose uzima wa milele.

●Wewe Mchungaji wa kondoo ambaye badala ya kuchunga kondoo wewe unatafuna kondoo mmoja mmoja wasio na akili.

■Usipobadilika utaenda jehanamu hata kama kwa sasa unaitwa mzee wa Kanisa au shemasi au kiongozi wa vijana au kiongozi wa wamama au Mwalimu wa kwaya au mwanakwaya au Mwalimu wa watoto.

■Usipotubu na kuacha uchafu wako ujue siku ile YESU Mwokozi atakuambia kwamba hakukujua kamwe.

●Wewe Mchungaji unayetangaza Kanisani kwamba unaenda mbali kufanya huduma kumbe unaenda kwa hawara yako.

●Enyi wanakwaya ambao mmegeuzana chakula kila mwanakwaya.

MUNGU amenituma nisema na inawezekana hii ndio nafasi yako ya mwisho umepewa.

Kuna makanisa ni zaidi ya danguro.

Kuna makanisa ni zaidi ya chuo cha kujifunza ukahaba.

Kuna makanisa uzinzi na uasherati uko kiwango sawa na kwa wapagani.

1 Wakorintho 5:1 " Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye."

●Kuna wamama wachungaji ni wazinzi na huwasaidia mabinti wa Kanisa kutoa mimba.

Kuna mabinti walishawahi kutoa hadi mimba za watumishi.

Ndugu, ni wakati wa kujikana na kujipambanua hata kama wanakwaya wenzako wote wameoza kwa uasherati na uzinzi.

Wewe usifanye dhambi hizo.

Ni wakati wa kujipambanua hata kama wabinti wenzako Kanisani ni waasherati.

Ndugu, kumbuka Neno la MUNGU linasema Wagalatia 6:5 " Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe."

Wengine watabeba mafurushi yao kwenda jehanamu na sio mbinguni.

Wewe mtoto wa Mchungaji wala hutaenda mbinguni kwa sababu baba yako au babu yako ni Mchungaji au Askofu.

Ndugu, umepewa nafasi ya kutubu wewe binafsi, ukiichezea nafasi yako ujue watu wa aina yako wataenda jehanamu.

Kuna watu wako Kanisani hata miaka zaidi ya 10 lakini watu hao hawajawahi kuwa kondoo bali wao ni mbuzi tu siku zote, ndugu kuna jehanamu ya moto kwa waovu.

Nilipewa maandiko manne kwa ufunuo huu ili mwenye sikio la kusikia asikie Leo na kuacha dhambi zote hasa uzinzi na uasherati.

Neno la MUNGU mwenyezi linasema

Ufunuo 2:11 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili."

Ufunuo 2:29 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."

Ufunuo 3:22 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."

Ufunuo 3:6 "Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa."

Mimi nimekuambia Leo.

■Yule aliye na sikio la kusikia asikie Leo na kuacha uzinzi na uasherati.

●Kuna watu wengi sana wakiwa jehanamu wataaanza kuwalalamikia wachungaji wao kwamba kwanini hawakuwaonya wala kuwakemea, watawalaumu wachungaji wao kwa nini walihubiri mafanikio tu na sio toba.

Ndugu uliye wa Kanisa Mimi najua ni neema ya MUNGU mwenyewe ili ujifunze ujumbe huu kisha uache uzinzi na uasherati.

Mimi Peter Mabula ninamshukuru Bwana YESU maana alichoniambia kusema nimesema.

"Asante Eee Mwokozi wangu YESU KRISTO.

Mwenye sikio la kusikia atatubu na kuacha uzinzi na uasherati kuanzia Leo."

Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.

MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
Bwana YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na Bwana YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee Bwana YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
By Mwl Peter Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
+255714252292(chochote na WhatsApp)
Ubarikiwe

Comments