WAKO WAITWAO MUNGU ILA KWETU MUNGU NI MMOJA TU.

 

Na Mwl Peter Mabula 
Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi 

Bwana YESU KKRISTO atukuzwe ndugu zangu wote.

Karibuni  sana tujifunze Neno la  MUNGU.


◾Katika ulimwenngu wako  miungu wengi sana na watu  wengi  huwatambua na  kuwaabudu, ni  ubatili  na  upotovu  mkubwa sana.


➡️Hata ukisooma Biblia wako miungu wengi sana kama  akina Dagoni, Baali, Ashera,  Mooleki,Milkom, Baal-zebuli,nisrok, Rimmon n.k

Hiyo  yote nii miungu na  ni maroho wa kuzimu.


Miungu hii  sio MUNGU ndio  maana MUNGU  wa kweli  anaweza kuiadhibu.


Kutoka 12:12 "Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; NAMI NITAFANYA HUKUMU JUU YA MIUNGU YOTE ya Misri; Mimi ndimi BWANA."


 ◼️Ingawa miungu ni wengi sana  lakini MUNGU wa kweli ni  mmoja  tu na Biblia  inatupa siri  yake kwa  usahihi.


1 Wakorintho 8:5-6 " Kwa maana ijapokuwa wako waitwao miungu, ama mbinguni ama duniani, kama vile walivyoko miungu mingi na mabwana wengi; lakini KWETU SISI MUNGU NI MMOJA TU, ALIYE BABA, AMBAYE VITU VYOTE VIMETOKA KWAKE, NASI TUNAISHI KWAKE; YUKO NA BWANA MMOJA YESU KRISTO, AMBAYE KWAKE VITU VYOTE VIMEKUWAPO, NA SISI KWA YEYE HUYO."


◼️MUNGU  wa  kweli ni mmoja  tu na  yuko  na  Mwanaye wa pekee  YESU KRISTO.


➡️Hakuna Mwanadamu  yeyote hata  mmoja anayeweza kumfahamu MUNGU wa kweli nje  na  KRISTO YESU.


Yohana 1:18 "Hakuna mtu aliyemwona MUNGU wakati wo wote; MUNGU Mwana pekee aliye katika kifua cha BABA, huyu ndiye aliyemfunua."


◼️Hivyo  kama  kuna  mtu yeyote  duniani anadhani ana Mungu wa kweli nje na MUNGU katika  KRISTO YESU jibu  ni kwamba mtu huyo  ana   miungu.


➡️Leo duniani kuna dini  zaidi ya 15 na watu  wengi  ni waumini wamefuata dini hizo, ukweli mmoja  ni  kwamba watu wote wa dini zote zilizo  nje  na Wokovu wa  KRISTO YESU, Watu hao wanaabudu  miungu na  sio MUNGU.


Matendo  4:12 "Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo."


➡️Leo kuna  madhehebu  maelfu ya dini mbalimbali, ukweli mmoja  ni kwamba  kila  dhehebu au madhehebu yaliyo  kinyume na Wokovu wa  KRISTO, mtu huyo  anahusika huko  anaabudu  miungu na sio MUNGU wa Mbinguni.


◼️Bwana  YESU alisema  aliyemuona yeye huyo ndie amemuona MUNGU  wa kweli  mmoja.


Yohana 14:9 "YESU akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe BABA?"


◼️◼️Hiyo  ina maana  kila anayemfuata YESU huyo  ndiye anayemfuata MUNGU wa kweli.


◼️Ndugu, unayemfuata YESU KRISO wewe  umemfuata MUNGU wa kweli.


◼️Ukimuona YESU umemona MUNGU wa kweli.


Yohana 14:7 "Kama mngalinijua MIMI, mngalimjua na BABA; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona."


➡️Ndugu amua kuanzia leo kujitenga na miungu maana MUNGU wa kweli  umemfahamu.


1 Yohana 5:20 "Nasi twajua kwamba Mwana wa MUNGU amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake YESU KRISTO. Huyu ndiye MUNGU wa kweli, na uzima wa milele."


➡️Ndugu, hata  kama  dini yako ni nzuri  sana, ina  mafundisho mazuri, ina tamaduni nzuri kama dini hiyo iko kinyume na  Wokovu wa KRISTO YESU hiyo  dini ni ya shetani, ondoka kwenye dini ya shetani.


1 Timotheo 4:1 "Basi ROHO anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;"


◼️Ndugu amua kumpokea YESU KRISTO kama Mwokozi wako kuanzia leo.

Ndugu amua kuokoka ili sasa uanze kuumwabudu MUNGU wa kweli.


Yohana 4:23-24 " Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu BABA katika roho na kweli. Kwa maana BABA awatafuta watu kama hao wamwabudu. MUNGU ni ROHO, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."


➡️Kumbuka miungu ni wengi ila MUNGU ni mmoja.


Je  wewe hadi sasa uko  kwa MUNGU au kwa  miungu?


◼️◼️Nakushauri njoo kwa YESU  KRISTO.


Asante kwa kujifunza Neno la  siku ya leo, Kabla sijamaliza nakuomba Wewe ambaye hujaokoka au uliokoka ukarudi nyuma, nakusihi sana amua Leo kumpokea YESU KRISTO kama Mwokozi wako na Jina lako litaandikwa katika kitabu Cha uzima Mbinguni, katika maeneo Yako tafuta Kanisa safi la kiroho linalohubiri Wokovu wa KRISTO YESU nenda kamweleze Mchungaji atakuongoza Sala ya Toba utaokoka Kisha baada ya hapo fuata mafundisho ya Neno la MUNGU hapo Kanisani.

MUNGU wa Mbinguni akubariki sana.

By Mwl Peter Mabula 

Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi.

+255714252292 ( kwa Ushauri, maombezi,  pamoja na Whatsapp)

Ubarikiwe

Comments