MTUMISHI WA MUNGU OMBA MUNGU AJIFUNUE KWAKO BINAFSI.

 

Na Mwl Peter Mabula 
Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi 

Bwana YESU KRISTO Mwokozi atukuzwe rafiki.

Karibu Tujifunze Neno la MUNGU.

➡️Ukisoma Hesabu 12:6 Biblia inasema " Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi, BWANA,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto." Hiyo maana yake MUNGU anaweza akajifunua kwa Mtumishi wake yeyote hapa ametoa Mfano wa kujifunua kwa Nabii na ukiendelea  kusoma Hesabu 12:8 Biblia inasema Kwamba MUNGU Kwa Musa atajifunua tofauti na anavyojifunua kwa manabii, Biblia inasema "Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?"


◼️Kama Kuna kitu Muhimu sana kwa Mtumishi wa MUNGU katika KRISTO YESU basi ni MUNGU kujifunua kwa Mtumishi huyo binafsi, maana Kila Mtumishi katika Mwili wa KRISTO ana jukumu lake.


Zaburi 98:2 "BWANA ameufunua wokovu wake, Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake."


➡️Mfano MUNGU ameufunua Wokovu wake kwa watu wote lakini Watumishi wote sio Wainjilisti Wala sio Wachungaji Wala sio Mitume na Wala wote sio Manabii, omba MUNGU ajifunue kwako binafsi ili ujijue Wewe ni nani.

Namshukuru MUNGU wa Mbinguni Mimi  Bwana YESU aliponiita alijifunua kwangu hata nikajua Mimi ni nani na majukumu yangu katika kazi yake ni yapi.


◼️Kama MUNGU asipojifunua kwako utatembea kwenye Maono ya wengine.


◼️Kama Bwana YESU KRISTO asipojifunua kwako ni rahisi kukosea au kwenda nje na wito wako kwa kuiga wengine au kwa kutumia akili zako kinyume na kusudi la MUNGU Kwa wito wako.


◾Mimi  nimewahi kuwauliza maswali Wachungaji kadhaa juu ya ndoto walizoota Kila mara kabla hawajawa Wachungaji na nilijifunza kitu juu ya "wito binafsi wa Mtu"


➡️Mchungaji mmoja alisema hivi " kabla sijafungua Kanisa nikiwa tu nimeokoka nilikuwa naota Kila mara navua samaki na kuweka kwenye Tenga, ndoto nyingine naota navua samaki mtoni, ndoto zingine navua samaki ziwani na zingine navua samaki Baharini, ndoto za hivi zilikuwa zinajirudia mara nyingi." Mimi Peter Mabula Nikagundua Bwana YESU alipomuita alijifunua kwa Mtumishi huyo ili awe Mchungaji, hata Petro alifunuliwa na Bwana YESU aliponiitwa kwamba atakuwa mvuvi wa Watu.


Luka 5:10 "na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. YESU akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu."


◼️Hapa Bwana YESU alikuwa anajifunua kwa Petro juu ya huduma aliyomwitia yaani kuvua watu au kwa Jina lingine kuwatoa watu Duniani na kuwapeleka kwa MUNGU.


➡️Mchungaji Mwingine kabla ya kuanza Uchungaji akiwa tu Kijana aliyeokoka anayemcha MUNGU alikuwa anaota mara kwa mara akivua samaki katika ardhi ya eneo Fulani mkoa fulani, baadae alipata akili ya kwenda kuanzisha Kanisa katika eneo hilo jambo la ajabu alipoenda tu eneo hilo alipata watu wengi sana katika huduma yake, huduma yake ni kubwa hadi Leo ingawa eneo hilo na mkoa husika  aliloanzisha Kanisa ni eneo ambalo asilimia 95 ya wakazi wa eneo hilo ni dini nyingine nje na Ukristo.


◼️Mtumishi wa MUNGU omba sana MUNGU ajifunue kwako binafsi ili ujue wito wako.


➡️Mtumishi Mwingine aliota Ndoto mara kadhaa akiwa ameshika Biblia akitembea na watu wengi sana wakimfuata, baadae huyu akawa Mwalimu mzuri sana wa Neno la MUNGU Kwa mamilioni ya watu.


➡️Mtumishi Mwingine aliota akiwa ameshika fimbo na maelfu ya watu wakimfuata baadae alikuwa na ujumbe wa ajabu wa Maombi ya kuwatoa watu kwenye vifungo vya shetani na watu wengi sana wakafunguliwa.


◼️Bwana YESU kujifunua kwa Mtumishi wake Ina maana kubwa sana.


◼️MUNGU anaweza akajifunua kwako kukuonyesha Nini utafanya au Nini ufanye katika wito aliokuitia kwenye kazi yake.


Tito 1:3 akalifunua neno lake kwa majira yake katika ule ujumbe niliowekewa amana mimi kwa amri ya Mwokozi wetu Mungu;


◼️MUNGU anaweza akajifunua kwa kukupa maelekezo binafsi ya Wewe kwenye mwili wa KRISTO 


Mfano hai ni huu ambapo Amos alipewa huduma ya kuwaonya  watu na Wafalme hata wakawa hawataki atabili.


Amosi 7:14-17 " Ndipo Amosii akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu; naye BWANA akanitwaa, katika kufuatana na kundi; BWANA akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu Israeli. Basi, sasa lisikie neno la BWANA; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka; kwa hiyo, BWANA asema hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa kutoka nchi yake."


◼️Ndio maana Leno Lengo  la MUNGU ni kwamba watu waokoke waupate Uzima Wa Milele lakini Kila Mtumishi na Staili yake ya kuwafanya watu wampokee KRISTO YESU na kuokoka.


➡️Katika wito wengine ni waandishi wa vitabu, wengine huendesha semina, wengine mikutano ya Injili, wengine kushuhudia, wengine uumbaji n.k na Kwa njia hizo watu wengi wanakuja kwa YESU KRISTO.


Waefeso 4:1-7 " Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika BWANA, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa ROHO katika kifungo cha amani. Mwili mmoja, na ROHO mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

 BWANA mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. MUNGU mmoja, naye ni BABA wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote. Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake KRISTO."


➡️Wengine Bwana YESU amejifunua kwao wawe Mitume, wengine Manabii, wengine Wainjilisti, wengine Wachungaji na wengine Walimu.


◼️Kwa MUNGU Ziko idara nyingi sana, ni Muhimu sana kubaki Kila Mtumishi kwenye Idara yake aliyopewa na MUNGU wakati MUNGU anajifunua kwa Mtumishi huyo.


➡️Wengine mkazo wa Ufunuo waliopewa ni kuhubiri Imani, wengine kuhubiri Maombi, wengine kuhubiri utoaji, wengine kuhubiri ROHO MTAKATIFU n.k


◼️Lakini funuo zote hizo Lengo ni kuwafanya watu wawe ndani ya Wokovu wa KRISTO na waishi Maisha Matakatifu ya Wokovu.


 Asante kwa kujifunza Neno la  siku ya leo, Kabla sijamaliza nakuomba Wewe ambaye hujaokoka au uliokoka ukarudi nyuma, nakusihi sana amua Leo kumpokea YESU KRISTO kama Mwokozi wako na Jina lako litaandikwa katika kitabu Cha uzima Mbinguni, katika maeneo Yako tafuta Kanisa safi la kiroho linalohubiri Wokovu wa KRISTO YESU nenda kamweleze Mchungaji atakuongoza Sala ya Toba utaokoka Kisha baada ya hapo fuata mafundisho ya Neno la MUNGU hapo Kanisani.

MUNGU wa Mbinguni akubariki sana.

By Mwl Peter Mabula 

Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO Mwokozi.

+255714252292 ( kwa Ushauri, maombezi,  pamoja na Whatsapp)

Ubarikiwe.

Comments