Posted by
Peter Mabula
- Get link
 - X
 - Other Apps
 
![]()  | 
| MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE AKIFUNDISHA NENO LA MUNGU | 
![]()  | 
| DIANA MWAKASEGE AKIWAONGOZA WATU KWENYE KONGAMANO LA MAOMBI | 
 Siku moja usiku nikiwa katika chumba cha hoteli moja 
hapa hapa nchini, baada ya kutoka kwenye semina ya kiroho; Roho 
Mtakatifu alisema ndani ya roho yangu kuwa; “Fundisha juu ya Damu ya 
Yesu Kristo”.
 
                 Tangu wakati huo nimekuwa na 
maombi ya mara kwa mara, nikiomba Roho Mtakatifu anifundishe juu ya Damu
 ya Yesu Kristo. Nimekuwa nikisoma na kutafakari neno la Mungu 
linalofundisha juu ya damu ya Yesu Kristo. Ni muda umepita sasa tangu 
nipate agizo hili. Ndani ya moyo wangu naona ya kuwa muda umefika wa 
mimi kuanza kuwashirikisha wenzangu yale ambayo tayari yamo ndani yangu 
ingawa ni machache, juu ya Damu ya Yesu Kristo.
 
                 Katika mfulilizo wa somo hili,tutashirikiana juu ya 
mambo manne tunayopata katika Damu ya Yesu Kristo. Ukweli ni kwamba 
katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne 
nitakayokushirikisha humu; lakini kwa sasa naona nianze na haya manne:-
 
 1.       Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kuondoa dhambi. Imeandikwa
 katika kitabu cha 1Yohana 1:9 kuwa; “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni 
mwaminifu na wa haki hata ATUONDOLEE dhambi zetu, na kutusafisha na 
udhalimu wote”.
 
 2.       Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika 
kupatanisha. Imeandikwa katika kitabu cha Waefeso 2:13-16 kuwa; “Lakini 
sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa 
karibu kwa damu yake Kristo. Kwa maana yeye ndiye amanin yetu, 
aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza 
cha kati kilichotutenga. Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake;
 ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa 
mtu  mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. AKAWAPATANISHA wote
 wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha 
kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”
 
 3.       Uzima wa Milele 
katika Damu ya Yesu Kristo. Imeandikwa katika kitabu cha Yohana 6:53-54 
kuwa; “Basi Yesu akawaambia Amini, amini, nawaambieni, msipoula mwili 
wake mwana wa Adamu nakuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye 
mwili wangu na kuinywa damu yangu anao UZIMA WA MILELE…..”
 
 4.  
     Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kutulinda. Imeandikwa katika 
kitabu cha ufunuo wa Yohana 12:11a kuwa; “Nao wakamshinda (shetani) kwa 
damu ya mwana-Kondoo….”
 
 Mtihani mkubwa sana kwetu sisi wakristo
 ni kuyaweka katika matendo yale tunayofahamu katika Biblia. Nakushauri 
kwa Jina la Yesu Kristo kuwa uwe mtendaji wa neno, na usiwe msomaji tu.
 
 Ni maombi yangu kwa Bwana ya kuwa Roho wa ufahamu wa Bwana atakuwa juu 
yako. BARIKIWA SANA BY MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE 
- Get link
 - X
 - Other Apps
 


Comments