MATENDO 4:12 [WALA HAKUNA WOKOVU KATIKA MWINGINE AWAYE YOTE, KWA MAANA HAPANA JINA JINGINE CHINI YA MBINGU WALILOPEWA WANADAMU LITUPASALO KUOKOLEWA KWALO] YESU PEKEE NDIO ANA UZIMA WA MILELE
wala
hakuna wokovu katika mwingine awaye yote,kwa maana hapana jina jingine
chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo {MATENDO
4:12} Ndugu sijui kama unajua uzima wa milele. kama unautaka uzima wa
milele mpe YESU maisha yako.dunia itapita na mambo yake yote ndio maana
BWANA YESU alisema kwamba itamsaidia nini mtu akipata vitu vyote harafu
akifa aende motoni? ni wakati wa mimi na wewe kugeuka na kumpa YESU
maisha yetu awe BWANA na MWOKOZI wa maisha yetu hvyo hakuna haja ya
kusema nitaokoka tu ipo siku kwa sasa ngoja kwanza. Ndugu usidanganyike
kiasi hicho amua leo kufanyika mtoto wa MUNGU kwa kumpa YESU maisha
yako. Na ujumbe huu ni kwa ajili yako kwani sijaandika tu ili
kujifurahisha bali ni agizo la MUNGU kwangu leo hivyo MUNGU
aliyenifunulia hili akutie nguvu na kukusaidia kufikia kuokoka leo pia
shetani asikuhubiri chochote kile iwe ni kupitia ndugu,marafiki au
yeyote kwani hao hawana mbingu ya kukupeleka ila YESU pekee ndiye
atakupeleka uzimani na yeye alisema katika YOHANA 14:3 BASI MIMI
NIKIENDA NA KUWAANDALIA MAHALI ,NITAKUJA TENA NIWAKARIBISHE KWANGU ILI
NILIPO MIMI NANYI MWEPO.una heri wewe utakayemchagua BWANA YESU baada ya
kupata ujumbe huu na MUNGU wangu akubariki na kukushindia kwa kila
hatua ya wokovu AMEN. [HII IMETOKA KWENYE PAGE YETU YA www.facebook.com/maishaYaUshindi.]
Comments