NI TAMU ILA NI SUMU

Ayubu 20:12-13, 27

Ingawa UOVU una tamu kinywani mwake, Ingawa auficha chini ya ulimi wake, Ingawa auhurumia, asikubali kuuacha uende zake, Lakini akaushika vivyo kinywani mwake….. Mbingu zitafunua wazi uovu wake, Nayo inchi itainuka kinyume chake. 
 Ni hali ya kawaida katika ulimwengu wa maendeleo kuona vidonge hasa vya kutibu malaria kuona vimepakwa radha ya sukari kwa nje, lakini kwa ndani ni chungu ajabu. Siku moja niliona mtoto akilia baada ya kutafuna kidonge aina ya Comaquine ambacho alipolamba akaona ni kitamu akafikiri Pipi, baada ya kutafuna ndipo akakutana na Uchungu.  Ndivyo ilivyo kwa mitego ya panya, wengi wanaweka SUMU ndani ya Mchuzi wa Samaki au nyama, panya anapokula anasikia Utamu mpaka kwenye Kisogo, lakini baada ya muda mfupi utakuta amekufa bila matumaini.
Wewe kijana na rafiki yangu unayesoma tafakari ya leo, nataka nikuambie kuwa dhambi ni tamu lakini ndani yake Adui ameweka Sumu ambayo ni lazima itemize kusudi lake. Piga picha siku ulipokutana na huyo boy friend au girl friend wako, ukalegeza macho na kutamka neno “Honey / Sweet I LOVE YOU”  ulijisikiaje? Na hatimaye utakuta taratibu lakini kwa uhakika wanakokotana hadi wanaingia katika Dhambi ya Zinaa. Wengi hawapendi kuvunja Amri ya Mungu inayosema “USIZINI”, lakini kwa hila za shetani anawaangusha. Tendo la Ndoa nje ya Ndoa halali ni Dhambi ya Zinaa, hiyo ni sukari iliyotiwa sumu ya kufisha, inaua taratibu lakini kwa uhakika.  
Kijana mmoja aliyenusulika kufa akiwa amekunywa sumu ya panya akitaka kujiua baada ya kugundua ameambukizwa Virusi vya ukimwi, tulipomuuliza ilikuwaje? Akasema rafiki yangu wa kiume alinilazimisha kufanya naye ngono, siku moja alimtembelea boy friend wake, chumba chenyewe ni kimoja na viti ni kitanda, alipoingia, kwa maneno ya kubembeleza wakajikuta wamefika kwenye “Point of No Return” wakavunja AMRI sa saba, ndivyo vijana wengi walivyoanguka bila kutarajia na wanabaki wakisema “NINGEJUA” lakini wanakuwa wamechelewa.
Neno linasema, Dhambi ni TAMU na wengi wanajitahidi KUIFICHA ili wasigundulike, wasije wakaicha, Lakini Mungu anasema; Mbingu zitaifunua na  itawekwa wazi. Popote unapokuwa, iwe Guest House, Chumbani, kwenye vichochoro, hata iwe usiku wa GIZA nene, chochote unachofanya, Kamera ya Mbinguni inakumulika na kuchukuwa Picha, chicho la BWANA liko kila mahali likichunguza kila tendo – na mwisho anasema ATAUFUNUA UOVU HUO.
MUNGU ANATUFUTA VIJANA KAMA AKINA DANIEL KATIKA KIZAZI CHA LEO WATAKAOSIMAMA KWA UAMINIFU – KWA NINI USIWE WEWE?
SIKU YA LEO IKAWE YA BARAKA NA USHINDI TELE

Comments