Na Mtu wa Mungu Samson Mboya
Utangulizi: Wengi wetu tunapenda sana kufanya maombi ila kuna sababu
nyingi zinzoweza kuzuwia maombi yako yasijibiwe na Mungu mojawapo ya
sababu hizo nyingi katika somo langu nitaongelea sana kuomba kwa imani,
kila anayeomba maandiko yanatufafanulia na aombe kwa imani,
Yakobo 1:6, 7 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye
shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa
huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa
Bwana.
· Mashaka katika kuomba ni kama mtu mgonjwa anayejilazimisha
kufanya kazi ngumu,
· Mashaka ni kirusi cha kuharibu imani ya mtu
· Mashaka yanahamisha imani ilipo kupeleka sehemu nyingine
kwamfano kama ukona mchumba na Mungu alishakudhibitishia labda kwa ndoto
maono au kwa mjumbe kuja kwako kukamilisha uhakika huo, usipoamini kile
ulichoonyeshwa na mungu umeruhusu Roho nyingine ya kuja kuharibu imani
yako na hapo watu wengi huwa wanajikwaa sana ,
· Kama huwezi kuamini kupokea muujiza wako kutoka kwa Mungu basi
maishani mwako usitarajie jambo jema, maana hata ukiomba ni kama
unapoteza muda wako bure,
Isaya 45:11 Bwana, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi;
Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya
kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni. Wakati wote Mungu ameruhusu
tumuombe lolote ila kwa utaratibu alioufanya yeye mwenyewe, kile
unachokiomba ni kwaajili gani unakitaka je? Unataka kunyanyasa wengine,
au kuonekana kwa wengine au ni kwautukufu wa Mungu?
Yeremia 29:13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo
wenu wote. Mungu hajajificha sehemu nyingi alizosema nitafuteni
alimaanisha maisha yako umuhusishe Mungu kwa kila jambo kuonekana kwa
Bwana katika maisha yako ni wewe kumkubali atawale maisha yako yote,
*
Mathayo 21:21B, 21D, 22Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa
na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata
mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka. Na yo yote
mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.
1. Kuamini katika kuomba kuna maana kubwa sana mbele za Bwana
inaonyesha kumheshimu Mungu na kumtegemea yeye nayeye atatenda juu ya
hitaji lako,
Marko 11:24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali,
aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. Hakuna kinachoweza
kuwa chako katika ulimwengu wa Kiroho ikiwa hujaamini kuwa chako hivyo
kuchukuwa kitu chochote na kukimiliki katika ibada ya maombi ni kuamini
kwanza,
Luka 11:9, 10 Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi
mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa. Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye
atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. Wengi hukata tamaa sana
pale wanapoomba maombi yakichelewa na Muovu anafurahia sana kukwama
kukatakwako tamaa,
Warumi 4:20, 21 Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini,
bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu; huku akijua hakika ya
kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi. Imani si mtaji tu bali ni
nguvu ya kubeba kile unachokitaka,
Waefeso 3:20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno
kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi
ndani yetu;
Ø Kila unaloliomba omba kwakuamini unachokitaka,
Ø Omba kwaajili ya utukufu wa Mungu-si kwakumuonyesha mwanadamu
Ø Fahamu kwamba kila utakaloliomba kwa usahihi Litajibiwa na Bwana
Mungu
Ø Fahamu siri ya Maombi kisha angalia Mtu wa kumshirikisha si kila
mmoja anayetekiwa kufahamu unachokiomba Kwa Mungu,
Waebrania 4:16 Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili
tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji. Mungu
hajibu maombi kwaajili ya machozi au kwakukaa muda mrefu lah bali fahamu
si kwaakili zetu bali ni kwarehema zake Mungu
Waebrania 11:6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu
amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa
thawabu wale wamtafutao. Kabla hujaomba ukiwa unawaza kuomba Mungu
anakuona na ameshafahamu kusudio la Moyo wako, japo wewe inawezekana
usifahamu hivyo kabila ya kutamka maneno ya maombi unayoomba kwa Bwana
Mungu akiangalia Moyoni mwako anachokiona ni Mashaka na si imani huwezi
kupokea mahali hapa patakusaidia sana Mungu ametaka ujifunze kuomba
kwaimani Mimi ninaamini baada ya somo hili wewe utaanza kuomba kwa imani
Bila ya kukata tamaa, na utashuhudia wengine kile Mungu
alichokutendea,
Yakobo 1:6, 7 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye
shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa
huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa
Bwana.
Maombi yako yameambatana na machozi mengi kwasababu ya maumivu ambayo
hujui yataondoka vipi, mimi natakakukuambia baada ya kumaliza kusoma
ujumbe huu hautatumia nguvu kubwa sana wala machozi mengi kama
unavyoomba sasa bali utajikuta unaomba katika Roho na kweli, na
kwaimani,
1Yohana 5:14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu
sawasawa na mapenzi yake, atusikia.
Wahooo!! Sasa unaweza kuingia katika maombi ya imani pata muda wa
kutafakari kile unachotaka kukiomba usikurupuke tu kwakuwa umetingwa na
matatizo,Tulia na sema nakuona hujatulia, pata kikombe cha maji masafi
ya kunywa alafu jiulize unataka kuomba nini kwa Mungu na ni kwanini
unaomba, hilo hitaji, tatu unaomba na nani, Musa aliomba na Haruni,uri,
Eliya akaomba na Elisha, Yesu akatenga wanafunzi wakuomb naye wewe
unaomba na nani!?
Ikiwa hujui au ungetaka upatiwe mtu wa kukusaidia kuomba basi usihofu
Mungu ameona hitaji lako na amelijibu,
Umbali usikuzuwie kupata huduma pata Mtenda mmoja toka katika Hema ya
Kinabii naye atakusaidia au ukihitaji ushahuri kabla ya maombi piga simu
namba 0756 809 209 huduma hii ni bure kabisa ni kwaajili yako wewe
itapokelewa na Mtu wa Mungu
Comments