Tamasha la Pasaka:Mashabiki wa muziki wa Injili nchini wamependekeza mwanamuziki Solly Mahlangu 'Obrigado'
Mashabiki wa muziki wa Injili nchini wamependekeza mwanamuziki Solly Mahlangu 'Obrigado' kutoka Afrika Kusini awepo kwenye tamasha la Pasaka mwaka huu kwani mwanaumuziki huyo alifanya vizuri katika tamasha la Krisimasi mwaka jana.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Pasaka, Alex Msama alisema jana katika taarifa yake aliyoitoa kwenye vyombo vya habari kuwa wamepokea simu nyingi sana kutoka kwa wadau mbalimbali wa muziki huo wakitaka msanii huyo aalikwe katika Tamasha la Pasaka mwaka huu.
"Inaonekana Watanzania walifurahia sana kazi ya Solly Mahlangu mwaka jana, karibu kila anayepiga simu ya kupendekeza msanii, jina hilo lazima, sasa bado tunaendelea kupokea ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali, ambapo mpaka sasa Rebecca Malope na huyo Mahlangu wamekuwa wakipigiwa kura sana kwa waimbaji wa nje," alisema Msama.
Mahlangu ni muimbaji ambaye anashika kasi katika anga ya muziki wa Injili Afrika ambaye pia anamudu kuimba Kiswahili kizuri kwa baadhi ya nyimbo zake.
Mwimbaji wa muziki wa injili Solomon Mahlangu kutoka nchini Afrka Kusini akiimba jukwaani kwenye uwanja wa Taifa katika tamasha kubwa la Krismas lililofanyika jijini Dar es salaam likishirikisha waimbaji wengi kutoka nchi mbalimbali za afrika wakiwemo waimbaji wa Tanzania. |
Comments