MAANA YA MAJINA HAYA AMBAYO YANAPATIKANA KWENYE BIBLIA.( sehemu ya 2)




Farao = Nyumba kubwa

Festo = Mwenye sherehe


Filemoni = Mwenye upendo. Mkarimu


Filipo = Rafiki wa farasi. Anayependa farasi


Gabrieli = Mtu wa MUNGU


Gamalieli = Zawadi ya MUNGU. MUNGU anatoa thawabu


Gideoni = Anayepiga hadi kufa.


Haruni = Aliyeangaza. Anayeangaa


Hawa = Uhai.


Henoko =  Kuweka wakfu


Hezekia = MUNGU ni nguvu yangu


Hosea = Wokovu.


Ibrahimu = Baba wa wengi


Imanueli = MUNGU pamoja nasi


Isakari = Yeye anatoa ajira. Ananipa mshahara


Isaya = YAHWEH anaokoa. YAHWEH ni wokovu


Ishmaeli = MUNGU anasikia maombi


Israeli = MUNGU anapigana. Anapigana na MUNGU


Karmeli = Bustani (ya MUNGU)


Kornelio = Mwenye pembe


Lawi = Umoja. Nia moja


Lazaro = Eleasar = MUNGU ni msaada. MUNGU amesaidia


Lea = Aliyechoka. Mwenye nguvu. Malkia wa nyumba


Luka = Mwanga. Kuangaza


Lutu = Shera. Pazia


Magdalene = Anayetoka Magdala


Malaki = Malaika wangu. Mpeleka ujumbe


Manase = Yeye (MUNGU) amenifanya kusahau


Martha = Malkia


Mathayo = Zawadi ya YEHOVA


Melkizedeki = Mfalme wa busara, Mfalme wa Amani.


Mika, Mikaya = Nani kama YEHOVA


Mikaeli = Nani anayelingana na YEHOVA


Moleki = Mfalme


Musa = Anayevutwa juu


Naftali = Mapambano. Vita vyangu


Naomi = Uzuri wangu. Anayenipendeza. Mzuri


Nathanaeli = MUNGU ametoa


Nathani = Yeye (MUNGU) ametoa


Nehemia = YEHOVA anafariji


Nikodemo = Mshindi wa taifa

Nuhu = Mapumziko


Obadia = Mtumishi wa YEHOVA


Onesimo = Mwenye faida. Anayesababisha baraka

Kwa leo naishia hapo, itaendelea sehemu inayofuata, usikose.
na kama unataka kusomo maana ya majina yaliyopita FUNGUA HAPA


MUNGU akubariki sana  ni mimi ndugu yako Peter Michael Mabula Maisha ya ushindi Ministry 
0714252292

Comments