MADHARA YA KUANZISHA MAHUSIANO MAPYA WAKATI BADO UNA MAJERAHA NA VIDONDA VYA ALIYEPITA!




 Na Mchungaji Peter Mitimingi

Kabla ya kupanda mbegu mpya ya upendo kwa mtu, ni lazima mtu achukue muda wa kutosha kushughulikia na madondo na majeraha yaliyotokana na mahusiano ya nyuma na mtu aliyekuumiza au kukujurehi. 

Watu wengi hufanya makosa wakidhani kuwa njia pekee ya kupona dhidi ya majeraha ya maumivu yaliyopita ni kutafuta mtu mwingine katika mahusiano atakaye chukua nafasi ya yule aliyemsababishia kuumia. 

Hilo ni kosa ambalo badala ya kuleta faraja na upendo anaoutafuta atajikuta anajiumiza mwenyewe na kumuumiza mwenzake na pia yeye kuumizwa zaidi ya mara ya kwanza. 


Unashauriwa kabla hujaanzisha mahusinao na mtu mwingine ni lazima uwe na muda wa kutosha kupona madonda kwanza ndipo utakuwa na ndoa yenye baraka na amani.


Comments