REBECA MALOPE TAMASHA LA PASAKA 2014 DAR.


 MALKIA wa muziki wa Injili nchini Afrika Kusini, Rebecca Malope ni miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza kwenye Tamasha la Pasaka mwaka huu. 

Rebecca Malope

TAMASHA la Pasaka mwaka huu limetimiza miaka 14 tangu kuasisiwa kwake na Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam imekuwa ikijiongezea umaarufu na kukubalika zaidi kutokana na ubunifu wake wa kufanya maadhimisho ya Sikukuu za Pasaka na Krismasi kwa umahiri na mguso wa kiroho kupitia matamasha hayo.

Tamasha la pasaka la Mwaka huu litakalozinduliwa rasmi April
20,jijini dar likibeba kaulimbiu ya

 “Tanzania kwanza haki huinuaTaifa”

Msama alisema,maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na katika mazingira ya kwenda na wakati,limekuwa na kauli mbiu ya “Tanzania kwanza haki huinua Taifa”.


1
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama,

Miongoni mwa waimbaji waliotikisa tamasha la Krismas ambalo lilizinduliwa rasmi Desemba 25,mwaka jana jijini Dar,kabla ya kuhamia mikoani,


Ni Solly Mahlangu,



Ephrahim Sekereti,

Rose Muhando,





  Upendo Kilahirio

Upendo Nkone

 

Edson Mwasabwite

wengineo,wakiwemo vijana wa Acapella
a.k.a The Voice.

The Voice.

 

 Hapana shaka kuwa ubunifu huu ndio ulichangia hata Serikali kupitia Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenela Mukangala, kumteua Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama, kuwa Mjumbe wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)./

 

                     chanzo:Apostle darmacy blog

Comments