TAFSIRI YA NAMBA 4 KIBIBLIA



Na Mchungaji na Mwalimu Peter Mitimingi, Mkurugenzi wa Huduma ya The Voice of Hope Ministry(VHM)

TAFSIRI YA NAMBA 4 KIBIBLIA
Tumeuanza mwezi wa 4. 2014


Namba NNE ni namba ya uumbaji.


1. Katika siku ya NNE Mungu alikamisha kuumba vitu.

2. Kuna pande kuu NNE zinazokamilisha dunia, (Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi (Isa 11:12).

3. Katika Hekalu la Ezekiel kulikuwa na meza za sadaka NNE upande mmoja na NNE upande mwingine.

4. Siku imegawanyika katika sehemu NNE. (Asubuhi, Mchana, Jioni na Usiku).

5. Katika amri kumi, amri NNE zinahusisha zaidi juu ya dunia.

6. Injili NNE zinawakilisha maisha ya Yesu hapa duniani.

7. Wanawake wa-NNE wametajwa katika mlolongo wa kuzaliwa kwa Yesu. (Thamar, Rahabu, Ruth na Mke aliyekuwa wa Huria).

8. Kuna vijana wa-NNE wa-Kiebrania waliotajwa katika kitabu cha Daniel.

9. Kuna wafalme wa-NNE waliotajwa katika kitabu cha Dniel. (Nebukadineza na Belshashaza wa wafalme wa Babeli, wengine ni Dairo na Silas wa Uajemi).

10. Ezekieli inazungumza juu ya Hukumu NNE juu ya Dunia.

11. Vizazi vi NNE vilionwa na Ayubu kabla ya kufa kwake (Job 42:166)

12. Kambi ya waisrael iligawanyika katika sehemu kuu nne Hesabu 2:1-34

13. Baada ya Yesu Kutungikwa msalabani askari wa kirumi waligawanya vazi la Yesu vipande vine kila kipande kwajili ya kila mmoja wao. Yoh. 19:23

14. Kuna vipindi muhimu vinavyo ongoza majira katika dunia.(1. Fall 2. Winter 3. Spring 4. Summer)

15. Siku imegawanyika katika vipindi vine. (1. Asubuhi 2. Mchana 3. Jioni 4. Usiku)

16. Yesu alitoa mfano wa aina nne za Udongo. Mathayo 13.

Namba NNE ni namba ya uumbaji.
Ninamuomba Mungu katika mwezi huu wa 4 Aumbe jambi jipya katika mwezi huu uwe mwezi ambao utauma mafanikio na baraka katika maisha yako.

Comments