JIFUNZE TAFSIRI YA NAMBA 5 KIBIBLIA

Mchungaji Peter Mitimingi, mkurugenzi wa The Voice of Hope Ministries (VHM).

Namba TANO ni namba ya neema ya maajabu ya Mungu.
Nakutakia Neema na Maajabu ya Mungu katika MWezi huu wa 5

1. Mwanzo 1:20, 21 tunasoma udhihirisho wa neema ya Mungu katika kuumba. Aliumba viumbe hai katika siku ya TANO.
2. Katika Mwanzo 15:9, Mungu aliagiza wanyama WATANO wachinjwe.
3. Isaya 9:6 inamtaja Yesu katika nafsi TANO, (Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani).
4. Yesu aliwalisha watu zaidi ya elfu TANO na mikateilikuwa MITANO.
(Mt 15:13
5. Waefeso 4:11, Kristo alitoa huduma TANO kwa Kanisa. (Mitume, Manabii, Wachungaji, Wainjilisti na Waalimu.
6. Katika Mambo ya Walawi waliamriwa kutoa sadaka za aina TANO. (Sadaka ya Ondoleo la Dhambi, Sadaka ya Asili, Sadaka ya Matendo ya Dhambi, Sadaka ya Amani).
7. Kulikuwa na wanawali wa TANO wenye busara na WATANO wapumbavu
8. (Mt 25:34)
9. Namba TANO imetajwa mara 318 katika maandiko.
10. Amri 10 zimegawanyika katika mafungu mawili, amri TANO za kwanza zinazungumzia juu ya uhusiano wetu na Mungu, na amri TANO zingine zinazungumzia juu ya uhusiano wetu sisi kwa sisi.
11. Katika agano la kale mwizi lazima alipe mara TANO ya thamani ya mifugo aliyoiba.(Kutoka 22:1)
1 “Mtu akiiba ng'ombe au kondoo, na kumchinja, au kumwuza; atalipa ng'ombe watano badala ya ng'ombe mmoja, na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja”
Nawewe kila ambacho shetani ameiba mwezi huu lazima arudishe mara tano ya thamani yake sema amen.

13. Benjamin aliheshimiwa na Yusufu kwa kupewa nafaka mara TANO zaidi ya kaka zake. (Mwanzo 43:34)
“34 Wakapelekewa sehemu za chakula kutoka mezani pake, lakini akazidisha sehemu ya Benyamini iwe kubwa mara TANO kuliko zao. Wakanywa, wakafanya furaha pamoja naye.”

14. Namba Tano inawakirisha Neema ya Mungu na hii inaonekana katika muundo wa hema ya kukutania kule jangwani. (Kutoka Sura ya 26)
• Nguzo zilikuwa dhiraa TANO mbali na mikono mitano ya juu.

• Madhabahu ya shaba ilikuwa mikono MITANO kwa mikono mitano.

• Kulikuwa na nguzo TANO mwishoni mwa Patakatifu.

• Pande za maskani zilikuwa kushinikizwa na baa TANO kila upande (Kutoka 26:26-27)
Nawe fanya mataruma ya mti wa mshita; mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani, 27 na mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.

• Mfuniko wa ndani mwa hema ulikuwa na mapazia matano ambayo yaliambatanishwa na mapazia MATANO mengine na kufanya jumla ya mapazia 10. (Kutoka 26:3)
3 Mapazia matano yataungwa pamoja, hili na hili; na mapazia MATANO mengine yataungwa pamoja, hili na hili.”

• Kulikuwa na makuhani halisi watano Haruni na watoto wake wanne (Kutoka 28:1)
“Nawe umlete Haruni ndugu yako karibu nami, na wanawe pamoja naye, miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani. Haruni, na Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari, wana wa Haruni.”

15. Kulikuwa na Matao TANO katika lile birika la Bethaida. (Yohana 5:2)
2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano

16. Kitabu cha Zaburi kimegawanyika katika sehemu huu TANO
• Zaburi 1- 41
Inahusu sikukuu ya Pasaka, mwanzo wa Israeli, na mwanzo wa mpango wa Mungu wa wokovu kuelekea Kristo.

• Zaburi 42 – 72
Inahusu juu ya ishara ya umoja wa Israel katika ardhi na inatoa picha ya uumbaji wa kanisa la Agano jipya.
• Zaburi 73 – 89
Laana juu ya uharibifu wa hekalu la Mungu na mji wa Yerusalem. Sehemu hii pia inazungumzia juu ya siku za mwisho na dhiki kuu.

• Zaburi 90 – 106
Kufurahia zaidi ya 1,000 ya utawala wa Yesu na inaonyesha Israeli walikutana tena

• Zaburi 107 – 150
Inatoa picha ya wakati ambapo Yuda (mwakilishi wa Israel) atakapokombolewa tena.

KAMA UMEBARIKIWA SEMA AMEN!

Comments