WAIGIZAJI FILAMU WAFIKA KANISANI KUOMBEWA ULINZI.

Mchungaji Harris Kapiga akifundisha katika ibada hiyo.

Mchungaji Kiongozi wa Nchi ya Ahadi (Harris Kapiga ambaye pia ni mtangazaji wa Clouds Fm) siku ya jana katika ibada yake aliandaa maalumu kwaajili ya kuvunja roho za mauti kwa wasanii wa filamu nchini kutokana na roho ya mauti iliyowagubika siku za hivi karibuni ikishuhudiwa waigizaji watatu wakiaga dunia.
Maombi hayo pia yalikua maalumu kuwaombea ulinzi,umoja na wote wanaotamani kuingia katika tasnia ya filamu Tanzania. Ibada hiyo ya wasanii wa bongo movie iliwakilishwa na Rais wa shirikisho la filamu Tanzania (TAFF) Saimon Mwakifamba.wasani wengine waliofika pamoja na waimbaji Bahati Bukuku,Dotnata na Mfue na wengineo.

Bahati Bukuku akimwaibisha shetani kwa sifa kwa Mungu wake.

Mwigizaji ambaye pia ameokoka kwasasa mwanamama Dotnata akiwa uweponi.


Mama mchungaji Kapiga akifanya maombi kanisani hapo.

Samson Mwakifwamba akiwa katika hali ya maombi.

Bahati Bukuku akiwa kanisani hapo.
Picha na habari kwa hisani ya unclejimmytemu.com

Comments