Skip to main content
NILIONA JINI JUU YA MTI NA KUTAKIWA KUUANGAMIZA HUO MTI.
 |
|
Usidharau
Ndoto Unayoota. Mwaka 2009 Nikiwa Zanzibar. Mimi Na Rafiki Zangu 4
Tulipanga Nyumba 1 Kwa Wakati 1. Baada Ya Kuanza Maisha Pale Majirani
Walikua Wanatushangaa Na Tulipowauliza Wakasema Kwamba Nyumba Tuliyo
Panga Huwa Haikaliwi Na Watu Maana Ina Nguvu Za Giza Za Hatari Sana,
Hivyo Wanatushangaa Sana Na Siku Tunahamia Pale Tulikuta Godoro Na
Vyombo Viko Nje, Tukaambiwa Vitu Hivyo Amevikimbia
Mpangaji Mmoja Mpemba. Hatukuwa Na Wasiwasi Maana JEHOVAH Ndiye Mlinzi
Wetu. Maisha Yaliendelea Kama Kawaida Na Baada Siku Chache Kabla Hata Ya
Wiki Tangu Tuhamie Pale Niliota Ndoto Usiku Nikiona Miti Ya Machungwa
Miwili Ambayo Iko Nje Ya Nyumba Yetu, Ndani Ya Mti 1 Ambao Ulikua
Kushoto Nilimuona Njiwa Wa Kijani, Nikaambiwa Huyo Sio Njiwa Ila Ni
Jini, Natakiwa Kesho Yake Niende Kwenye Huo Mti Na Kukata Ka Tawi Kadogo
Sana Kisha Niombe Nikiuzunguka Huo Mti Nikisema " ENYI NGUVU ZA GIZA
NAWATEKETEZA KWA JINA LA YESU KRISTO" Kweli Kesho Yake Nikafanya Kama
Nilivyoelekezwa Ndotoni,Nikaomba Nikiuzunguka Ule Mti. Baada Ya Kuomba
Niliendelea Na Kazi Zangu Kama Kawaida. Baada Ya Siku 2 Tangu Nivunje
Nguvu Hizo Za Giza Kwenye Mti, Ule Mti Ulianza Kupukutika Majani Na
Baada Ya Wiki Mti Mzima Ulikuwa Umekauka. Wenzangu Hawakujua
Kinachoendelea, Baadae Kidogo Yule Mzee Baba Mwenye Nyumba Akaja Na
Kuanza Kutukana Akisema Kuna Mtu Mbaya Kati Yetu Na Ambaye Ameharibu
Vitu Vyake. Wenzangu Hawakujua Ila Siri Mimi Niliijua. Yule Mzee
Alifanya Uchunguzi Wake Wa Kipepo Na Kugundua Ni Mimi Ndio Nimeua Vitu
Vyake, Akawa Ananiogopa Sana Na Hata Kuniangalia Usoni Akawa Hawezi.
Baadae Alianza Visa Akisema Kwamba Niache Kuweka CD Za Gospel Kwenye
Redio Yangu Maana Zinamomonyoa Nyumba Yake. Pale Kama Kuna Mtu Alikua
Analiza Redio Kwa Sauti Ndogo Basi Ni Mimi Lakini Mimi Huyo Huyo Ndio
Nageuka Adui. Baada Ya Kodi Yangu Ya Chumba Kuisha Yule Mzee Alikataa
Nisiongeze Kodi Bali Nihame Kwenye Nyumba Yake. Nikahama, Ndugu Yangu
Usidharau Ndoto Unayoota Bali Husika Nayo Kwa Maombi Kwa Jina La YESU
KRISTO.
Baadhi ya ndoto nazifahamu maana zake nitakuwa nakuletea ili ujue ufanyeje maombi.
Ubarikiwe.
Kwenye
Ndoto Ukiota Uko Barabarani Na Unaongozwa Na Askari Na Kuamrishwa
Sehemu Ya Kwenda Na Ukakubali, Hiyo Ni Ndoto Mbaya, Maana Yake Adui Zako
Wanakusimamia Na Kukuongoza Kila Mahali Kuhusu Mipango Yako. Haribu
Mipango Hiyo Ya Uovu Kwa Kutumia Jina La YESU KRISTO, Kwenye Maombi
Tumia Ufunuo 12:11, Zaburi 62:11-12, Yohana 8:36 Na Mathayo 12:37.
Lakini Ukiona Kwenye Ndoto Unakataa Kuwatii Askari Mkiwa
Barabarani, Hiyo Ni Ndoto Nzuri, MUNGU Anakupa Ushindi Juu Ya Maadui
Zako, Mshukuru BWANA Na Endelea Na Maombi Ukitumia Zaburi 35 Na Zaburi
140. Lakini Ukiota Askari Mkiwa Barabarani Analazimisha Kwa Nguvu Nawe
Ukamuua, Hiyo Nzuri, Una Nguvu Za MUNGU, Mshukuru MUNGU Na Endelea Na
Maombi, Tumia Yakobo 4:7. BWANA YESU Anakupenda Sana Na Anakuwazia Mema
Sana.
Kwenye
Ndoto Ukiota Unamuua Paka Ni Ndoto Nzuri. Maana Yake MUNGU Amekuwezesha
Kuwafukuza Adui Zako, Mshukuru MUNGU Na Endelea Na Maombi Katika ROHO
MTAKATIFU. Tumia Wafilipi 2:10:11
Kwenye
Ndoto Ukiota Unalima Jangwani, Hiyo Ni Mbaya, Maana Yake Biashara
Unayoifanya Haitakupa Mahitaji Unayohitaji Katika Maisha Yako. Kataa
Hali Hiyo Kwa Maombi Ya Vita Kupitia Jina La YESU KRISTO Ukitumia
Mathayo 12:37, Isaya 41:10 Na Yeremia 15:21. MUNGU BABA Akubariki Sana
Na BWANA YESU Anakupenda Sana, Songa Nae Tu Hadi Uzima Wa Milele.
Kwenye
Ndoto Ukiota Mtu Anakupa Yai Lililopikwa, Ni Mbaya, Maana Yake Adui
Zako Wamekutegea Mtego Mbele Yako Kwa Njia Ya Chakula, Unatakiwa Kuwa
Mtulivu Na Kufunga Mdomo Wako Kwa Ajili Ya Kujilinda, Ondoa Hasira Na
Ufunge Na Kuomba Kuharibu Mipango Hiyo Ya Maadaui Zako. Omba Maombi Ya
Vita Ukitumia Waefeso 6:12, Yeremia 23:29, Mithali 18:21, Zaburi 50:15
Na Isaya 48:17. MUNGU Akubariki Sana Na BWANA YESU Anakupenda Sana,
Songa Mbele Na Yeye Milele Yote.
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU Akubariki.
Comments