BWANA YESU
asifiwe!
Karibu
ujifunze kitu hapa ambacho kitakusaidia kuweza kufuta laana za kukuzuia kuolewa/kuoa.
Laana ni
kitu kinachokushika ili usifanye jambo Fulani jema.
Laana ni
mfano wa ndege aliyefungwa kamba ndefu mguuni kwenye mti , hutoka na kupaa
karibu tu na kurudi kwenye mti , hawezi kwenda zaidi. Na mtu mwenye laana ya
kutokuolewa/kuoa hupata mateso makubwa sana . Ni kama yuko huru lakini
kuchumbiwa/kuchumbia ni mtihani, na hata
akichumbiwa/Kuchumbia kabla ya kuolewa/Kuoa uchumba unavunjika, au akiolewa tu
anaachika au mme/Mke anakufa kifo cha
ghafla cha mapema. Kuna haja ya kujifungua kutoka kwenye laana zote ikiwemo laana
ya kutokuolewa/Kuoa. laana hii katoa nani? Yawezekana adui za wazazi wako,
yawezekana mababu katika ukoo, yawezekana wachawi, yawezekana maadui wa ukoo
wako , yawezekana maadui wa familia yako, yawezekana majini mahaba ya ndotoni,
yawezekana waganga wa kienyeji, yawezekana ni mizimu au shetani mwenyewe na
yawezekana mtu yeyote mwenye nia mbaya na ukoo wenu au nia mbaya na familia
yenu au nia mbaya na uzao wa tumbo la mama yako na wewe ukiwamo ndani yake.
Unaweza
kuepuka laana au mikosi ambayo ni kisababisho
cha mateso wakati wa kuoa/kuolewa kama mmoja kati ya wanaooana yuko
kwenye mkondo wa laana.
NJIA
KUMI(10) ZA KUTAMBUA KAMA UNA LAANA YA KUTOKUOLEWA.
1.
Ukiwa
na ndugu wa kike zaidi ya wawili wakubwa, wenye miaka 30 na zaidi, ambao
hawajawahi kuchumbiwa kabisa.
2.
Kila
unapokaribia kuolewa katika zaidi ya matukio mawili, mara zote huishia
kukatishwa tamaa na uchumba wako kuvunjika bila sababu za kueleweka.
3.
Endapo
kuna hali inayoashiria kifo cha ndoa, na ambayo huharibu ndoa kabisa.
4.
Hata
kama ni mwanamke mzuri na mwenye mwenendo mzuri na maisha ya maadili mema,
utaona kabisa hakuna kijana anayevutiwa na wewe ili kukuchumbia muoane. Hata kwa wale wenye
nia ya kukuchumbia hujikuta wakitoweka tu bila sababu.
5.
Endapo
Baba au Mama yako , au mtu mwingine akitoa laana ya maneno kuhusu wewe kuolewa.
6.
Ikiwa
msichana yeyote katika familia yako kaolewa katika mazingira magumu au wale
ambao hufa vifo visivyoelekea tena muda mfupi tu baada ya kuolewa.
7.
Endapo
utasikia sauti ikisisitiza kukuambia kuwa ‘’Kamwe hutaolewa’’ au ‘’Kamwe
hutapata mafanikio kwenye maisha yako.’’
8.
Ikiwa
una pepo mume au watoto wa kipepo. Kwa
mfano katika ndoto unazoota utaona mwanamume akija na kufanya mapenzi na wewe,
au kujiona una ujauzito na hatimaye kuzaa watoto katika ulimwengu wa roho yaani
katika ndoto. Wakati mwingine , mtu huyo anaweza hata akajidhuhirisha katika
ulimwengu wa Mwili.
9.
Kama
hupati kabisa siku zako za mwezi(Hedhi).
10.
Kama
wewe huota ndoto zenye kuogopesha hususani kuota unacheza na nyoka au viumbe
wenye kutambaa.
JINSI YA KUFUTA LAANA .
Kama ukigundua kuna laana katika
maisha yako.
1.
Hatua inayofuata ni wewe kwenda kufanyiwa maombezi.
2.
Kukutana na mtumishi aliyeokoka ambaye atakuongoza kwenye maombi yanayohusiana na ukombozi na
tatizo lako litaisha kwa jina la YESU KRISTO.
3.
Marko 16:15 YESU KRISTO anasema ‘’Na ishara hizi zitafuatana nao
waaminio, Kwa jina langu watatoa pepo’’
4.
BWANA YESU anaendelea kusema ili kuondoa ushetani huu katika maisha yako
anasema katika Luka 10:19 ‘’ Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge,
na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. ‘’
5.
Okoka na baada ya hapo tumia hata siku 3 za kufunga na kuomba maombi ya
nguvu, huku ukijiambatanisha na MUNGU huku ukifukuza kila aina ya mapepo na
kuharibu mamlaka yao inayofanya kazi katika maisha yako, haribu kwa jina la YESU KRISTO.
6.
Kuhusu majini mahaba yakatae na kwa jina la YESU KRISTO. Na bila huruma
muombe ROHO MTAKATIFU ashushe moto na kuharibu masalia ya majini mahaba.
7. Epuka mawazo ya ngono na badala yake
akili yako ijazwe Neno la MUNGU pamoja na nyimbo za kuabudu.
- Kila siku funika kitanda chako kwa
Damu ya YESU KRISTO kwa njia ya maombi.
8. Dumisha utakatifu na uwe mwana maombi
siku zote, omba katika ROHO MTAKATIFU na tumia mamlaka ya YESU KRISTO kujiweka
huru siku zote.
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
Comments