Na Mtumishi Peter M Mabula. |
BWANA YESU
atukuzwe ndugu zangu.
Karibu
tujifunze imani ya ushindi.
Imani ya
ushindi chanzo chake ni kulisikia neno la KRISTO.
Warumi 10:17
‘’ Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la KRISTO. ‘’
Imani ya
ushindi lazima ije kutokana na neno la KRISTO maana KRISTO ni mshindi na neno
lake lina ushindi wa milele. Mara nyingi sana BWANA YESU alisema ‘’Amini amin
nakuambia’’ maana yake alichokisema ni kweli na hakuna kweli zaidi ya ile kweli
aliyoisema BWANA YESU.
Yeremia 1:8
‘’ Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema BWANA .
‘’
Jambo ambalo
watu wengi hawajui ni kwamba imani ina macho. Ndio, imani ina macho na inaona.
Stephano alipokuwa anapigwa mawe aliona mbinguni na akamuona BWANA YESU akiwa
ameketi katika kiti cha uweza. Aliona kwa maono lakini maono hayo yaliambatana
na imani. Isingekuwa imani ya ushindi angesema ‘’wananipiga huku macho yangu
yananidanganya’’ lakini Macho ya imani yaliona na kusema ‘’Wala usijali maana
ukiondoka hapa duniani utaenda paleeeeee juu alipo BWANA wako YESU maana
aliahidi anakwenda kukuandalia makao, hivyo makao yako wala sio hapa ila
mbinguni’’
Imani
iliona.
Ayubu licha
ya kuwa katika wakati mgumu sana wa majaribu makuu lakini bado alisema
‘’
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama
juu ya nchi. Na
baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu
nitamwona MUNGU; Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama,
wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu. –Ayubu 19:25-27’’
-Imani ya
Ayubu aliona ushindi mkuu hata kama wakati huo ushindi haukuwepo. Macho ya
kawaida ya Ayubu hayakuona kwamba kuna kumuona mtetezi alie hai lakini macho ya
imani ya Ayubu yalimuona BWANA aliye
mtetezi aliye hai. Macho ya Imani ya Ayubu yalimuona BWANA akija kumsaidia,
kumponya na kumbariki upya na ndivyo ilivyokuja kuwa Biblia inasema
‘’ Basi hivyo BWANA akaubarikia huo mwisho wa
Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, na ngamia
elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu, na punda wake elfu. Tena alikuwa na wana waume saba, na
binti watatu. - Ayubu 42:12-13 ‘’
Imani ya
ushindi husema hivi;
=Nitashinda
na zaidi ya kushinda kwa YESU anayenishindia, BWANA atanishindia wala
hatanyamaza maana ninamuomba na kumuabudu katika kweli yake.
=MUNGU BABA
akiwa upande wangu, ni nani aliye juu yangu?
Warumi 8:31
‘’ 1 Basi,
tuseme nini juu ya hayo? MUNGU akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? ‘’
-Ni ugonjwa gani uli juu yangu?
- Ni laana gani
iliyo juu yangu?
- Ni shida gani iliyo juu yangu?
-Ni mchawi
nani aliye juu yangu?
- Ni mganga gani aliye juu yangu?
=Ni nani
atakayenishitaki mimi mteule wa MUNGU?
Warumi
8:33 ‘’ Ni nani atakayewashitaki wateule
wa MUNGU? MUNGU ndiye mwenye kuwahesabia haki. ‘’
-Mimi sitendi dhambi, je maneno ya watu ya
uongo yanishitaki na kunishinda?
-Sina hatia, je chuki za wafanya kazi wenzangu
ndizo zinishinde na kunirudisha nyuma?
-Haiwezekani maana hakuna
atakayenishitaki na kuniweza ikiwa MUNGU ndiye aliyesihesabia kuwa sina hatia
hata moja.
=Ni nani
atakayenihukumia adhabu?
Warumi 8:34
‘’ Ni nani atakayewahukumia adhabu? KRISTO YESU ndiye aliyekufa; naam, na zaidi
ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa MUNGU; tena ndiye
anayetuombea. ‘’
-Ni mchawi nani
akayetumia tunguli zake ili nife wakati Damu ya YESU inanilinda na ninaomba
kila siku?
-Ni nani atakayenitegea jinni njiani ili jinni liniue wakati BWANA
YESU ndiye anayenilinda?
=Ni nani
atakayenitenga na upendo wa KRISTO?
Warumi 8:35
‘’ Ni nani atakayetutenga na upendo wa KRISTO? Je! Ni dhiki au shida, au adha,
au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? ’’
-Je kaa njaa kanaweza kuonondoa kwa YESU?
- Je kukusa kazi dada ndiko kunaweza
kukuondoa kwa YESU kwa wewe kuamua kuwa kahaba?
- Je kukosa mchumba ndiko
kukuondoe kwa YESU ndugu?
Hapana, ukiwa na imani ya KRISTO ya ushindi hakuna
ambacho kinaweza kukuondoa katika Wokovu wa BWANA YESU.
Ndugu yangu,
Imani ya ushindi huwa haishindwi ila lazima ujue jinsi ya kuitumia.
Imani ya
ushindi hushindana kiroho na sio kimwili.
-kila jambo
chanzo chake ni katika ulimwengu wa roho. Hakuna jambo hata moja ambalo hutokea
katika ulimwengu wa mwili bila kwanza kutokea katika ulimwengu wa roho. N ahuko
katika ulimwengu war oho ssi MUNGU ametupa kumiliki na kushinda kila jambo
ambalo liko upande wa adui.
Warumi 8:37-39 ‘’ Kwa maana nimekwisha kujua
hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka,
wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini,
wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa MUNGU ulio
katika KRISTO YESU BWANA wetu.
‘’
-Tunashinda
kwa maombi makali kupitia jina la YESU KRISTO.
-Wakati
mwingine BWANA hutuonyesha yale yanayopangwa na maadui zetu katika ulimwengu
wa roho, BWANA hutuonyesha kwa njia ya ndoto na maono, hatutakiwi kudharau bali kuwadhibiti maadui
zetu huko huko katika ulimwengu wa roho kabla hawajafika katika ulimwengu wa
mwili.
Ndugu yangu
tumia fomula hii kwa njia ya maombi ili kuharibu maadui zako uliowaona katika
ulimwengu wa roho,
Yeremia
1:10‘’ angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na
kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda. ‘’
=KUNG’OA
=KUBOMOA
=KUHARIBU
=KUANGAMIZA.
Kisha
unajenga ufalme wa MUNGU kwa kutamka ushindi kwako kupitia jina la YESU KRISTO.
Panda uzima kama unaumwa, panda Baraka kama Baraka kwa maombi, panda ushindi
kupitia jina la YESU KRISTO. Ulipomfukuza adui usipaache wazi bali panga jambo
jema, Kama umemung’oa pepo mchafu ndani yako basi panda neno la MUNGU kwa
kulisoma sana. Panda uzima.
-Jambo la
kujua katika maombi ni kwamba sio kila adui ni wa kubomoa na sio kila adui ni
wa kung’oa na sio kila adui ni wa kuharibu na sio kila adui ni wa kuangamiza.
Ndio maana ROHO MTAKATIFU hutusaidia katika kuomba itupasavyo, hivyo hakikisha
unajazwa nguvu za ROHO MATAKTIFU. Hakika unaishi maisha matakatifu. Na kama
jambo umeliona kwenye ndoto lazima MUNGU akupe ufahamu wa kujua. Maana unaweza
kumuona mtoto mdogo kwenye ndoto analia, sio ukianza kuomba unang’oa, hata
sijui utang’oa nini. Ndio maana ROHO MTAKATIFU ni muhimu sana katika maisha
yetu maana mtoto uliyemuona anaweza kuwa ni mtu Fulani mahali Fulani anahitaji
maombi yako na msaada wako, umemuona rohoni lakini hakika atakuja katika
ulimwengu wa mwili na utamuona. Unaweza kumuona jirani yako anakupiga na ukajikuta unapambana na jirani huo kiroho
na kimwili kumbe kwenye ndoto ile ilikuwa ni taarifa tu kwamba kuna roho za
kipepo za kuonea zinakuja na anza kupambana na madhabahu hizo ili zisifike na
kuanza kukonea kazini, nyumbani na kokote utakakokuwa. Penda kupambana na roho
inayomtumikisha mtu na sio kupambana na mtu huyo, pambana na madhabahu
inayomtumia mtu huyo mbaya na sio kupambana nae, pambana na kiti cha enzi
alichokalia mtu huyo na sio kupambana nae lakini pia kama utatakiwa kupambana
nae basi pambana ila sio kimwili bali kiroho.
Yuda 1:20-23
‘’ Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na
kuomba katika ROHO MTAKATIFU, jilindeni katika
upendo wa MUNGU, huku mkingojea rehema ya BWANA
wetu YESU KRISTO, hata mpate uzima wa milele. Wahurumieni wengine walio
na shaka, na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine
wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili. ‘’
-Kaa katika
imani ya ushindi, funga na kuomba, omba katika ROHO, Vaa silaha za MUNGU ili
uweze kushinda. Silaha za MUNGU ambazo unatakiwa uzivae ni
=Neno la
MUNGU.
=Utakatifu.
=Dirii ya
haki na n.k.
Waefeso
3:20-21 ‘’ Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote
tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam, atukuzwe katika Kanisa na katika
KRISTO YESU hata vizazi vyote vya milele
na milele. Amina. ‘’
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio
kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na
utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi
kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments