ROHO YA DHULUMA


Na:     BRYSON LEMA (RP)        &

Dr. GODSON I. ZACHARIA (SNP)

Utangulizi: Imeandikwa katika MITHALI 13:23…[Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini;  Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.].. Biblia inasema chakula kipo kingi kwa mkulima lakini vipo viharibuvyo. Leo unafanya kazi zako kwa nguvu kubwa lakini matokeo ya kile ulichofanya hayaji kama ulivyotegemea kwa sababu wapo wanaokudhulumu. Adui zako kila kukicha wanaangalia ni jinsi gani wanaweza kukudhulumu, na ndio maana maisha yako hayawezi kwenda vizuri na kile unachokitegema huwezi kukipata kwa sababu adui ambaye ni “roho ya dhuluma” anataka uharibiwe.

MWANZO 6:11…[Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma.]…Biblia inasema kuwa “Dunia ikaharibika, na dunia ikajaa dhuluma” na kila mwenye mwili amejiharibia njia yake. Hapa Mungu aliona dunia imeharibika maana binadamu wamejaa dhuluma na hawawazi kujitafutia vya kwao bali wamekaa ili wakuharibie na kukudhulumu, lakini leo tutawapiga kwa Jina la Yesu.

Maisha tunayoishi leo si kama tunavyofanya kazi, kwa sababu hiyo maisha yetu yanakuwa magumu kila siku.Tumefanya mambo mengi kwa bidii lakini tumepokea tofauti maana matokeo yamekuwa madogo maana yupo adui anayefanana na mchwa maana anasubiri uwekeze yeye aharibu.
Inawezekana umeomba Mungu uongezewe mshahara, lakini baada ya kipato kuongezeka ndipo unaona matatizo mapya yanakuja maana yupo adui wa kukudhulumu ambaye anaamka maskini na jioni anakuwa tajiri. Hii dunia imejazwa na dhuluma maana msingi wa Shetani katika dunia amejenga katika kudhulumu, maana yeye Shetani yupo kwa ajili ya kuharibu, kuchinja na kuiba.
ZABURI 55:1-8…[Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.2 Unisikilize na kunijibu, Nimetanga-tanga nikilalama na kuugua.3 Kwa sababu ya sauti ya adui, Kwa sababu ya dhuluma yake yule mwovu. Kwa maana wananitupia uovu, Na kwa ghadhabu wananiudhi.4 Moyo wangu unaumia ndani yangu, Na hofu za mauti zimeniangukia.5 Hofu na tetemeko limenijia, Na hofu kubwa imenifunikiza.6 Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.7 Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.8 Ningefanya haraka kuzikimbia Dhoruba na tufani.]… Tunaona Daudi anamwendea Mungu kwa kuomba maana aliiona dunia kwa wakati wake imejaa dhuluma. Kwa sababu ya dhuluma hii Daudi akasema hofu ya mauti imemzunguka maana yake wako tayari kumwua. Daudi kutokana na kudhulumiwa akaona kama angekuwa na mabawa angeruka kama tai aende mbali ili asikae karibu na wale wanaotaka kumdhulumu.
Tunaona tatizo la Daudi lilianza pale alipopakwa mafuta. Na matatizo hayo yalianza kwa kasi, na yalianza mara alipomwua Goliathi na hapo ndipo mfalme akataka kumwua Daudi, badala ya kumsifia Daudi kwa kitendo chake cha kumsaidia mfalme kumwua Goliathi. Inawezekana hata wewe kwenye maisha yako kutokana na bidii yako kazini, bosi wako badala ya kukusifu kwa uchapakazi wako lakini badala yake atainua vita juu yako maana anakuwa anahisi labda utachukua nafasi yake. Unapoonekana una bidii tayari wanaanza kukufuatilia na vita inaanza maana wameona kitu ndani yako. Lakini mtu aliye mvivu hutaona akifuatiliwa wala kuinuliwa vita. Huu ni mwaka wa kumiliki, kutiisha na kutawala, hivyo ni lazima kuwapiga wanaokudhulumu na lazima warudishe vitu  vyote walivyo viiba. Inawezekana umeibiwa afya, kazi, ndoa n.k, vitu hivi unaweza kudhulumiwa kwa sababu wanaweza kukuwekea afya, kazi au ndoa bandia.
Kwa kadiri dunia inavyoongeza maarifa na Shetani naye anaongeza maarifa. Na hivyo dunia hii inahitaji wapambanaji wanaosema hapana sikubali. Saa imefika ukakatae hayo magonjwa na matatizo ya kwamba hapana mimi sikuumbwa hivyo. Wapo walioibiwa akili na watoto wamekuwa wa kifeli mitihani.
ZABURI 55:9-14…[Ee Bwana, uwaangamize, uzichafue ndimi zao, Maana nimeona dhuluma na fitina katika mji.10 Mchana na usiku huzunguka kutani mwake; Uovu na taabu zimo ndani yake;11 Tamaa mbaya zimo ndani yake; Dhuluma na hila haziondoki mitaani mwake.12 Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione.13 Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.14 Tulipeana shauri tamu; na kutembea Nyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.]…  Daudi hakuachia pale akasema anayeniletea dhuluma ni rafiki yangu sana ambaye tulipeana ushauri na tuliingia nyumbani mwa Mungu pamoja. Ina maana kwamba hadi kanisani wapo wanaodhulumu. Kanisani pamefika mahala kuwa si mahali pa watu kujengwa bali watu kulalamika.
Saa ndio hii kanisa la kweli lionekane nalo litaonekana kama wewe utasimama na kumpiga adhulumuye. Kanisani hatuji kwa ajili ya kuombewa bali ili Mungu atusaidie. Unapoenda kanisani ni lazima kanisa likufanye ubadilike. Kanisa linaanza na wewe mwenyewe na si mtu mwingine hivyo ni lazima umpige yule akudhulumuye. Wapo watu waliodhulumiwa kwenye akili, unaweza ukamwona kama mtu lakini ndani amewekewa akili ya mnyama. Ni afadhali ukutane na Simba usiku unaweza ukamkwepa, lakini si kukutana na binadamu wakati wa usiku.  Ndio maana tuona watu wameweka mbwa katika nyumba zao ili kujilinda na wanadamu. Utaona wapo watu wanaoweza kujilipua wenyewe ili kuwadhuru wengine, uwe na uhakika watu hao ndani yao si watu bali ni kitu kingine.
Jambo lolote unaloliona limetokea ujue ipo nguvu ya rohoni iliyosababisha jambo hilo kutokea. Dunia inapoelekea ni kwenye hatari na hivyo ni lazima uamke usingizini maana Shetani anataka kuleta madhara makubwa katika kudhulumu. Mfano tunaona ipo ndege ambayo ilianguka na hata unywele mmoja haukoonekana,” HII HAIWEZEKANI”. Shetani hapa alipofika hatuwezi kumwondoa kwa ibada ya siku moja bali inatupasa kuingia ndani sana na kuweza kumpiga. Ni muhimu uwe mtu wa kufanya ibada si kanisani tu bali hadi nyumbani. Na hii ni Saa ya Ufufuo na Uzima duniani ni saa ya kupeleka msingi mwingine katika dunia hii, ni saa ya kuvunja vunja nguvu za Shetani. Saa imefika na saa ndio hii kanisa limeinuka na misingi imeiunuka, ni saa yako ya kuinuka na ni saa ya waganga wa kienyiji kuondoka Tanzania. Ni saa ya kila kilichoibiwa kurudishwa. Acha kupewa moyo na amani tuliyonayo, amani hii ni utumwa na hivyo ni lazima tupigane safari hii. Ni saa ya kuangusha misingi ya uovu.  Hatuikubali hiyo amani maana wanakula wengine. Je! Amani hiyo ipo wapi?
Unapookoka ndiyo kazi inaanza maana ndipo watu wanainuka kukupinga. Lakini ukiokoka na kustarehe hutaona ukipingwa.Unapoona nyumba imejengwa ujue umechimbwa msingi na nyumba ndio ikasimama. Ukitaka usimame hapo ulipo ni lazima uchimbe umpige Shetani na baada ya hapo hakuna atakaye kupinga nawe utasimama juu. Unapochimba dhahabu kuna jiwe ambalo lazima ulipasue kwa baruti vingenevyo huwezi kupata dhahabu. Hivyo nawe ni lazima umpige Shetani, na usikubali kufarijiwa kwa kuambiwa Bwana atatenda, bali utake Bwana atende.
ZABURI 55:21…[Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi.]…Mdhulumaji haji kwa ghafla bali anakuotea. Ni saa ya kupambana sikubaliani na vitu vinavyoendelea katika maisha yangu,  nataka mabadiliko, na mabadiliko hayo si ya Taifa nataka mabadiliko yangu.
ZABURI 10:15…[Uuvunje mko

no wake mdhalimu, Na mbaya, uipatilize dhuluma yake, hata usiione
.]…Anasema aneyekudhulumu mkono wake uvunjwe. Kila mkono ulionyooshwa mahali popote uvunjwe kwa jina la Yesu. Wakuvunja mkono huo ulionyooshwa si mwingine bali ni wewe.
ZABURI 55:15…[Mauti na iwapate kwa ghafula, Na washuke kuzimu wangali hai, Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.]..Daudi anasema  wanaokudhulumu mauti iwapate, maana biblia inasema usimwache mwanamke mchawi aishi.
Ni lazima uokoke ili uweze kupata kibali cha kuvunja mkono ulionyooshwa juu yako na vitu vyako.

Comments