MOJA WAPO YA DALILI YA MZAZI ANAYETUMIA MABAVU KULEA WATOTO WAKE UNAJITAHIDI KUDHIBITI TABIA YA MTOTO

Na Mchungaji Peter Mitimingi.

Badala ya kuwafundisha watoto waweze kujidhibiti wenyewe, wazazi wanaokuwa wanalea kwa kutumia nguvu huwa wanataka kuwadhibiti watoto wao. Watoto wankuwa na nafasi ndogo na uchaguzi mdogo kujaribu kujifunza heshima zao wenyewe. Wanakuwa wanatilia mkazo katika kufuata kanuni bila hata ya kuwepo kwa aina yoyote ya ubunifu wa heshima na utii.
Watoto kama hawa wanapoendelea kukua wanakuwa na tabia kama zifuatazo:


1. Ukali kupita kiasi
2. Kuwa na misimamo mikali isiyo na tija wala msingi wowote.
3. Kama ni mke, anakuwa ni mke anayependa kumtawala mumewe kwa kutumia nguvu zaidi ya makubaliano.
4. Kama ni mume pia anakuwa ni mume anayependa kumtawala mkewe kwa kutumia nguvu zaidi ya makubaliano.
5. Mtoto huyu atakapokuwa mzazi atawalea watoto wake vile vile au hata zaidi ya jinsi wazazi wake walivyokuwa wakiwalea kimabavu.
6. Hatakuwa na maamuzi yake binafsi atategemea maamuzi ya wengine zaidi.
7. Mara nyingi maamuzi yake hayatakuwa sahihi atafanya maamuzi yasiyo sahihi mara kwa mara.


 

Comments