MAOMBI YA KUFUTA UCHAWI ULIOWAHI KUFANYIKA KATIKA MAISHA YAKO.

Na Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu.
karibu tujifunze Neno la MUNGU kisha tuombe maombi ya ushindi katika damu ya YESU KRISTO.
Maombi yetu yatahusu mambo matatu yafuatayo;
1. Maombi ya kufuta uchawi wa kutamkiwa.
A. Kutamkiwa wewe binafsi.
B. kutamkiwa uzao, iwe ni mababu au wazazi wako waliorogwa kwa kutamkiwa kisha uchawi huo ukakuathiri na wewe uliye sehemu ya uzao wao.
2. Maombi ya kufuta uchawi uliopitishiwa kwenye vitu kuja kwenye mwili wako.
3. Maombi ya kufuta uchawi kupitia ardhi.

Kutoka 22:18 '' Usimwache mwanamke mchawi kuishi.''
Kabla ya yote naomba ujue maana ya uchawi na mchawi.
Uchawi ni nini?
Uchawi ni ufundi wa kutumia dawa ili kuleta madhara.
Uchawi ndio usihiri, Uchawi ndio urogaji na ndio juju.
Kuroga maana yake ni kuzuru kwa kutumia uchawi
Mchawi ni mtu anayeweza kuwadhuru watu  kwa njia ya kuwaroga
 Kuna watu wengi sana wameathiriwa na uchawi katika maisha yao.
Kuna watu walirogwa zamani lakini madhara ya uchawi ule yapo hadi leo katika maisha yao.
Leo tunafuta uchawi wote uliowahi kufanyika zamani kutuhusu.
Tunafuta madhara ya uchawi yaliyotamkwa kutuelekea sisi.
Biblia ikataza uchawi na inakataza mwanadamu mwenye akili timamu kuwaendea wachawi na waganga.
Walawi 19:31 '' Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msiwatafute; ili kutiwa unajisi na wao; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.''
MUNGU anakataza uchawi maana ni kitu kinachoweza kumnajisi mtu.
Uchawi ni dhambi na uchawi ni uadui kwa MUNGU.
Mkristo hatakiwi kuwa mchawi.
Uchawi ni machukizo makuu.
Wachawi wapo sana na wanaroga sana lakini ashukuriwe MUNGU kwa kutupa jina la YESU KRISTO lililo kiboko ya wachawi wote na uchawi wao.
Biblia inathibitisha kwamba wachawi wapo na hutenda kazi zao mbovu za kichawi.
 Nahumu 3:4 ''Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.''
  
Kuna watu wamewahi kurogwa fahamu na akili zao zamani lakini hadi sasa hawajawahi kupona vyema.
Kuna watu biashara zao zimewahi kurogwa, uchumi na vipato vyao na hawajawahi kupona katika hayo, Leo uchumi wako utapona, biashara yako itapona na kipato chako kitapona kwa jina la YESU KRISTO.
Kuna watu wamewahi kurogwa afya zao ndio maana  hadi sasa hupona magonjwa kwa muda tu kisha magonjwa yale yanarudi, Ndugu leo kuna kupona katika jina la YESU KRISTO.
Kuna watu uzao wa tumbo zao ulirogwa na walikuja kuzaa uzao uliorogwa yaani walipata watoto waliofungwa kipepo.
Kanisa la MUNGU nin lazima lijitenge na uchawi.
Kanisa la MUNGU ni lazima likemee uchawi.
Zamani wachawi walikuwa wanauawa kwa mawe ndivyo Biblia isemavyo, Leo tunauua uchawi ndani ya wachawi kwa njia ya maombi yetu.
Leo malaika wa MUNGU wako tayari kupeleka mapigo kwa wachawi wote waliotusumbua, na kama walikendelea na uchawi huo basi tunamuomba MUNGU  wetu awaponde kupitia maombi yetu na damu yao itakuwa juu yao.
Walawi 20:27 ''Tena mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu yao itakuwa juu yao.''
 MUNGU wetu yuko tayari kutushindia leo dhidi ya wachawi wote waliofunga maisha yetu.
Leo kwa jina la YESU KRISTO maisha yetu yanaenda kuwa huru.
JEHOVAH MUNGU wetu anasema  '' Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema BWANA wa majeshi.-Malaki 3:5''
 Kuna ukoo huwa wanazika kila mwaka kwa sababu tu ya maneno ya mchawi aliyoyatamka zamani kwa ukoo ule.
Kuna watu nyoka hutembea katika miili yao.
Kuna watu fahamu zao zimefungwa katika mafundo ya uchawi.
Leo kila fundo la uchawi linapasuka kwa jina la YESU KRISTO.
Kuna watu miguu yao imerogwa kiasi kwamba hata waende wapi hawawezi kufanikiwa.
Kuna watu mikono yao imerogwa hata wafanye kazi gani hakuna kufanikiwa kiuchumi.
Biblia inasema kwamba kwa sababu hiyo ya uonevu wa shetani na wachawi wake ndio maana Bwana YESU alikuja ili tu kuziharibu kazi zote za shetani wakiwemo na wachawi.
1  Yohana 3:8 '' atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.''
Hakikisha leo kazi zote za uchawi zilizowahi kufanyika zikikuhusu, hakika zinaharibika na kutoweka.
YESU KRISTO alithihirishwa ili azivunje na kuzifuta kazi zote za shetani.
Leo futa uchawi wote uliowekewa kwenye uti wako wa mgongo.
Leo futa kwa damu ya YESU KRISTO kila uchawi ulifanyika kuhusu tumbo lako.
Leo hakikisha uso wako hautumiki tena kichawi, utakase uso wako na hakikisha uchawi hauharibu kibali chako tena.
Leo ni siku ya kushinda kama ukiomba katika jina la YESU KRISTO.

Leo futa uchawi wa kutamkiwa uliowahi kutamkiwa, Futa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Leo futa laana zote zilotamkwa na mchawi kwa wazazi wako au wazazi wa wazazi wako na laana hizo zimekupata na wewe,  leo Futa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
 Leo futa uchawi wote uliowekwa kwenye vitu ili uchawi huo uupate mwili wako, futa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Futa uchawi wote uliotamkwa katika ardhi yeyote inayokuhusu.
Siku napata ufunuo wa somo hili nilifuta kila uliofanyika katika ardhi ambayo mimi Peter nimewahi kukanyaga, Kila mabaya yanayonena mabayo kuhusu mimi yaliyo katika ardhi ambako nimewahi kukanyaga nilifuta kwa jina la YESU KRISTO na kwa damu ya YESU KRISTO, nilitaja mikoa hadi wilaya maana mawakala wa shetani hutumia sana ardhi ili kuwafunga watu wa MUNGU.
Leo ni siku moja ya kushinda katika jina la YESU KRISTO kama ukiomba katika kweli, katika imani na katika utakatifu autakao MUNGU.
MUNGU akubariki sana na usikose kukunua kitabu changu cha MAOMBI YA KINA ambacho kimeshachapwa na kinasubiri tu kuwekwa wakfu kwa maombi siku chache zijazo na baada ya hapo kila mtu atakipata.
Ukipenda pia kunisapoti kwa sadaka yako nakukaribisha sana ili sadaka hiyo inisaidie katika uinjilisti.
Maombi haya chini naomba yamsaidie muombaji mchanga katika kuliendea hitaji lake mwenyewe. Kwa waombaji wazoefu naamini kabisa baada tu ya kusoma somo umeandika maeneo ya kuombea na utaomba maana ni siku ya ushindi. Nasubiri pia shuhuda maana MUNGU Baba atatenda muujiza leo katika jina la YESU KRISTO.
Baada ya kuomba maombi ya kutubu na kuacha dhambi omba maombi haya chini.

  MAOMBI YA KUFUTA UCHAWI ULIOWAHI KUFANYIKA KATIKA MAISHA YAKO.

 Katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Ninafuta kila uchawi uliotamkwa kunihusu mimi, naufuta huo uchawi na naharibu madhara yake kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila mchawi aliyenitamkia nikiwa nasikia au hata nikiwa sisikii, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila uchawi ulionenwa njia panda au dirishani mwa chumba changu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
 Kila neno la siri la kichawi alilolitamka mchawi wa aina yeyote kunihusu mimi, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila mchawi anayeitamkia maneno mabaya ndoa yangu, uchumba wangu, biashara yangu, uzao wangu au masomo yangu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila mchawi anayenitamkia kifo au kuumwa au ajali au kufukuzwa kazi,  Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
 Kila mchawi aliyenena uchawi kuhusu mababu zangu zamani au wazazi wangu na uchawi huo unafuatilia maisha yangu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
Ninafuta kila kazi ya wachawi iliyofanyika zamani katika uzao wa babu yangu au wazazi wangu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
 Kila laana ya mchawi iliyotamkwa ili inipate, leo napangua kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila majanga yaliyokusudiwa kichawi, kiba balaa zilizopangwa kichawi, kila ajali zilizopangwa kichwi, leo nakataa kwa jina la YESU KRISTO na Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
 Kila uchawi uliotegwa kwenye vyakula au nguo zangu ili nidhurike, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
Kila uchawi nilioukanyaga na sasa unanitesa, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
Kila uchawi uliowekwa vitu nilivyonunua, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila nguo yangu iliyoibwa kichawi leo naichoma moto kwa damu ya YESU KRISTO huko iliko na kuanzia leo hakuna antena ya mchawi itaniona.
Kila kiungo cha mwili wangu, kila kucha au nywele au nguo za ndani vilivyotumika kichawi, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila uchawi uliowekwa katika mwili wangu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
Kila kiungo cha mwili cha bandia kilichopandwa na wachawi ndani ya mwili wangu, Leo nakifuta kitu hicho kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila uchawi uliowekwa kwenye vitu nilivyopewa kama zawadi, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
 Kila uchawi ulitegwa katika ofisi yangu au kiti changu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Sasa pia nafuta kila uchawi unaonena katika ardhi, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO
Najua kabisa damu huwa haifi hivyo damu za wanyama zilizomwagwa katika ardhi zikiambatana na maneno ya laana kwangu, Nazifuta leo damu hizo kwa damu ya agano ya YESU KRISTO.
 Kila mchanga uliowahi kuhukuliwa kwenuye nyayo zangu na ukatumika kichawi kunifunga,
Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
Kila uchawi wa aina yeyote uliofanyika popote kunihusu mimi au ndoa yangu au uzao wangu au familia yangu au ukoo wangu, Leo naufuta uchawi huo kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO.
 Nakushukuru MUNGU BABA maana umenipa ushindi kupitia damu ya YESU KRISTO aliye hai.
Naamini nimeshinda katika kilaeneo la Miasha yangu lililokuwa limefungwa kichawi.
Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea ushindi.
Amen Amen.

Asante kama umelielewa Neno la MUNGU ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Umeshashare sana jumbe zisizo na maana leo
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.

Comments