KITABU:MAOMBI KWA KINA.

Mchungaji Elly Botto akionyesha kitabu baada ya kukuweka wakfu kwa maombi. Wenye sare ni Mwinjilisti Peter Mabula na mkewe Scholar Mabula.
Siku jumapili tarehe 10 April 2017 ilikuwa ni siku ya Uzinduzi wa Kitabu cha kwanza cha Mwinjilisti Peter Mabula  Kiitwacho MAOMBI YA KINA.
Uzinduzi wa kitabu hicho ulifanyika katika Ukumbi wa Kanisa la Pentecostal Assemblies of GOD (P A G) tawi la kawe jijini Dar es salaam.
Katika ibada hiyo ya uzinduzi wa kitabu, Mchungaji Kiongozi wa Kawe Pentecostal Church Elly Boto alisoma maandiko kama utangulizi.
Maandiko aliyosoma ni kutoka Ayubu 22:27-28 Ambapo Biblia inasema  '' Utamwomba yeye(MUNGU) naye atakusikia; Nawe utazitimiliza nadhiri zako. Nawe utakusudia neno, nalo litathibitika kwako; Na mwanga utaziangazia njia zako.'' 
Baada ya Neno hilo lilifuata tukio la kukiweka wakfu kitabu hicho kwa maombi na kisha watu kuanza kukinunua.
Sasa kitabu hicho kinapatikana kwa Bei ya Tsh 8000  tU, wasiliana na Mwinjilisti Peter Mabula  kwa namba 0714252292 au 0786719090 kwa ajili ya kukupata.
Ubarikiwe.

Hizi hapa baadhi ya picha katika matukio ya siku hiyo ya uzinduzi wa kitabu hicho cha MAOMBI KWA KINA.

Mchungaji Elly Botto akisalimiana na Scholar Mabula

Peter na Scholar Mabula

Mchungaji Elly Boto akionyesha kitabu kwa waliohudhuria

Watoto wakielezea vifungu vya Biblia waliojifunza.

Mwandishi wa Kitabu cha MAOMBI YA KINA, Mwinjilisti Peter Mabula akikielezea kitabu hicho.

Watumishi wa MUNGU wakifuatilia kwa makini.

Viongozi wa Kanisa wakifuatilia

Mchungaji Botto akisoma maandiko ya Ayubu 22:27-28 kama sehemu ya utangulizi.

Wakati wa kukata utepe ili  kuzindua kitabu





Baada ya utepe kitabu kikawa wazi kwa kila mtu.

Pongezi kutoka kwa watumishi wa MUNGU.

Hongera

Scholar Mabula akimkabidhi Isa Danda baada ya kununua kitabu

James Onyango kutoka Kenya alikuwepo katika uzinduzi na kununua vitabu viwili.

Sarah Emmanuel akikabidhiwa kitabu chake baada ya kununua

Watumishi wa MUNGU baada ya kununua kitabu.





Ndugu Ilomo Kutoka akikabidhiwa kitabu baada ya kununua

Marry Baada ya kununua kitabu na kukabidhiwa na Scholar Mabula.

Comments