Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU. |
Bwana YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU kisha tuombe maombi ya ushindi.
Neno vazi
lina maana ya kitu chenye kuvaliwa.
Kibiblia
kuna aina mbili za Neno vazi
1. Vazi
linaloonekana mfano Mwanzo 3:21 '' BWANA Mungu akawafanyia Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.
''
2. Vazi
la kiroho ambalo halionekani kwa macho ya kawaida ila matokeo ya vazi hilo
huonekana, mfano Warumi 13:14 '' Bali mvaeni Bwana YESU KRISTO, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake.
''
Ukiangalia tafasiri ya BHN juu ya andiko hilo Biblia inasema
kwamba ‘’Bwana YESU awe vazi lenu’’
Kwa jinsi gani tumvae KRISTO?
Wagalatia 3:27 inajibu kwa kusema ‘’Maana ninyi nyote mliobatizwa katika KRISTO mmemvaa KRISTO.‘’
Tena 1 Petro 1 :15 inajibu kwa kusema ‘’ bali kama yeye(YESU) aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;‘’
Vazi la KRISTO ni vazi jema sana.
Lakini pia kuna vazi baya kiroho ambalo mtu anaweza akavikwa
kutoka ulimwengu wa roho wa giza, vazi hilo ndilo tunataka tupambane nalo leo
kwa jina la YESU ili litoke katika miili ya watu ambao MUNGU amewakusudia
ukiwemo wewe kama ulivalishwa vazi hilo la giza ili likutese.
Ni damu YESU KRISTO pekee inayoweza kuliondoa vazi hilo la
giza kwa maombi kupitia jina la YESU KRISTO.
Tutashinda leo kwa jina la YESU KRISTO kama ambavyo ROHO
MTAKATIFU ametupa ufunuo huu muhimu wa maombi.
Inawezekana bado hujaelewa, ngoja nikupe ushuhuda huu.
Mchungaji mmoja ambaye mimi Peter huwasiliana naye mara kwa
mara alikaa miaka mingi sana bila
kuumwa, hakuwahi kulazwa na ana miaka mingi sana sana bila kunywa dawa yeyote.
Kuna wakati mwaka jana
aliumwa sana hali iliyopelekea kwenda Hospitali, alikutwa anaumwa
magonjwa ya ajabu ajabu, mara kisukari, mara tatizo kwenye damu n.k. Kanisa
likaingia katika maombi. Siku hiyo hiyo mmoja wa wana Kanisa akaota ndoto kuona
Mchungaji wao amevikwa kipepo koti jeusi na akafunuliwa kwamba ili apone Kanisa
liombe kumvua hilo vazi la magonjwa alilovikwa. Kanisa lilipoomba maombi ya
kulivua vazi la kipepo hilo yule Mtumishi wa KRISTO alipona hakika na akaanza
kuhubiri injili kama kawaida maana alikuwa hana hata uwezo wa kusimama
madhabahuni tena.
Kwa hiyo kipepo wachawi au majini wanaweza kumvika mtu vazi
la kipepo ili limtese, unaweza kuvikwa vazi la kukataliwa, kuumwa umwa kila
mara, kudharauliwa, kuwa mtu wa hofu tu , kufuatiliwa na majini kila siku,
umasikini, mateso n.k
Ndio maana leo niko hapa kukuomba uombe maombi ya kufuta kwa
damu ya YESU kila vazi la kipepo ulilovikwa na mawakala za shetani.
Lakini kabla sijaendelea naomba kukupanua ufahamu juu ya vazi
kiroho.
1.
Wenye
dhambi wasiotubu kwa Bwana YESU watakwenda jehanamu kwa sababu kiroho watu hao
wamevaa vazi la kigeni yaani vazi wasilotakiwa kulivaa wanadamu walioumbwa na
MUNGU.
Vazi hilo la kigeni ni
dhambi.
Sefania 1:8 '' Na itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya Bwana, nitawaadhibu wakuu, na wana wa mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni.''
Vazi hilo hakuna
anayemvalisha mtu yeyote ila ni mtu mwenyewe kwa matendo yake ya dhambi
anajivalisha, kumpokea YESU na kutubu tu ndio njia pekee ya kulivua vazi hilo
la kigeni liitwalo dhambi ambalo halitakiwi kuwako katika wanadamu wanaoutaka
uzima wa milele. Ndugu livue vazi liitwalo dhambi ili lisiwe kamwe kwenye
maisha yako maana hilo ni vazi la kigeni yaani ni vazi baya kwako.
2.
Wokovu
wa YESU KRISTO ni vazi wanalotakiwa kulivaa watu wote duniani.
Isaya 61:10 '' Nitafurahi sana katika BWANA, nafsi
yangu itashangilia katika MUNGU wangu; maana amenivika mavazi ya
wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa
kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu.''.
Ndugu hakikisha unalivaa vazi hili muhimu sana.
Zaburi 132:16 '' Na makuhani wake nitawavika wokovu, Na watauwa wake watashangilia.''
3.
Maisha
ya haki katika KRISTO YESU ni vazi analotakiwa kulivaa kila mtu.
Ayubu 29:14 '' Nalijivika haki, ikanifunika, Adili yangu ilikuwa kama joho na kilemba.''
4.
Utakatifu
katika KRISTO ni vazi la wateule wa MUNGU.
Ufunuo 3:5-6 '' Yeye ashindaye atavikwa hivyo
mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima,
nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo ROHO ayaambia makanisa.
''. Ndugu hakikisha
unalivaa vazi hilo bila kulivua hata siku moja. Wakolosai 3:10 ''mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.
''
5.
Wito/Huduma
ni vazi kwenye ulimwengu wa kiroho.
2 Wafalme 2:9-15 ''...... Kisha akaliokota lile vazi la Eliya lililomwangukia, akarudi, akasimama katika ukingo wa Yordani.
14 Akalitwaa lile vazi la Eliya lililomwangukia, akayapiga maji, akasema, Yuko wapi Bwana, Mungu wa Eliya? Naye alipoyapiga maji, yakagawanyika huku na huku, Elisha akavuka. .......'''
14 Akalitwaa lile vazi la Eliya lililomwangukia, akayapiga maji, akasema, Yuko wapi Bwana, Mungu wa Eliya? Naye alipoyapiga maji, yakagawanyika huku na huku, Elisha akavuka. .......'''
Kama MUNGU amekupa
wito au huduma kwa ajili ya kazi yake katika
Kanisa la MUNGU hakikisha unatimiza wito wako na huduma yako.
Usikatae kufanya
kazi ya MUNGU. Usilivue vazi hilo wanalovaliswa na MUNGU wateule wake
waliookoka.
6.
Nguvu
za ROHO MTAKATIFU ni vazi la wateule wa KRISTO.
Luka 24:49 ''Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
''
7.
Vazi
safi la utakaso wa damu ya YESU KRISTO.
Zakaria 3:4 '' Naye huyo akajibu, akawaambia wale
waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha
akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi
ya thamani nyingi.
''.
Ndugu hakikisha
unamkimbilia Bwana YESU kwa ajili ya kutubu
na baada ya kutubu atakuvika vazi jipya la utakaso, hivyo utaanza kuwa
mtoto wa MUNGU na vazi la kwanza la dhambi malaika wataliondoa kwako maana sasa
utakuwa safi mbele za MUNGU.
Katika kitabu cha Ayubu
tunafahamu kwamba kwa kibali cha MUNGU na kwa sababu Maalumu MUNGU alimpa
kibali shetani amshambulie Ayubu(Hiyo ilikuwa kwa Ayubu tu hivyo usijenge Imani
yako kwamba unateseka kwa sababu MUNGU ametaka uteseke) Katika Maandiko anayemshambulia
Ayubu ni shetani na shetani alimshambulia Ayubu kwa magonjwa mabaya . Nataka
ujifunze kitu kwamba Ugonjwa unaopigana nao kipepo ni vazi.
Ayubu 7:5-6 ''Mwili wangu unavikwa mabuu na madongoa ya udongo; Ngozi yangu hufumba, kisha ikatumbuka tena.
Siku zangu hupita upesi kuliko chombo cha kufumia, Nazo zapita pasipokuwa na matumaini.
''.
Ayubu anakiri kwamba amevikwa vazi la ugonjwa.
Hata wewe wakuu wa giza
wanaweza kukuvika vazi baya hivyo maombi yako ya leo vua kila vazi la kipepo
ulilovikwa na mawakala wa shetani.
Kuna watu wamevikwa
mavazi machafu.
Zakaria 3:3 ''Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.''
Kuna watu watu wamevikwa
vazi la aibu,kudharauliwa, kuonewa, magonjwa, madeni, umasikini,ajali, matatizo
na kila uonevu.
Kuna watu kila akijaribu
kuomba kazi hapati lakini wengine wanajaribu
tu na kupata kazi, ndugu livue vazi la kipepo ulilovalishwa kwa
kutamkiwa kichawi na mawakala wa shetani.
Kuna waliovikwa kichawi
vazi la laana, kukataliwa, kuabishwa na kufeli katika maisha.
Kuna watu wamevikwa vazi
la kipepo la kuwafanya wawe chini tu.
Leo vua mavazi hayo ya
kipepo, yavue kwa damu ya YESU KRISTO kwa njia ya maombi.
Leo omba MUNGU ili
awavike wao vazi la aibu, kila mawakala
wa shetani wanaokufuatilia.
Livue na kulitowesha kwa
damu ya YESU KRISTO kila vazi la laana waliokuvika mawakala wa shetani.
Zaburi 109:18-29 ''Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake. Ikamwingilia moyoni kama maji, Na kama mafuta mifupani mwake.
Na iwe kwake kama vazi ajivikalo, Na kama mshipi ajifungao daima.''
Vua mavazi ya kipepo,
yavue kwa damu ya YESU KRISTO.
Mtu mmoja aliota ndoto akimuona mtu mwingine
akiwa kavalishwa kipepo makoti 7, yeye
hakujua lakini alipoona yule aliyemuona akiteseka katika mambo mengi
ndipo akamwambia na mimi wakanihusisha tukaomba ili kuyaondoa mavazi hayo ya
giza, ndipo matatizo yakaisha.
Kuna mtu kila
usingiziwaji na yeye yumo.
Kuna mtu kila balaa na
yeye yumo.
Ndugu leo kwa maombi
fuata kanuni hii.
1.
Yavue
mavazi ya kipepo yote uliyovalishwa.
2.
Yachome
moto kwa damu ya YESU KRISTO.
Pia katika maisha yako
yote usikubali tena usikubali haswaa vazi
lako la Wokovu likachakaa,
Ufunuo 7:14 ''Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka
katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe
katika damu ya Mwana-Kondoo.''
Hakikisha unalifua kila
siku vazi lako la Wokovu wa KRISTO ulio wa thamani sana. Fua vazi lako la
Wokovu kwa wewe kuishi maisha matakatifu kila siku, Kufanya maombi kila mara,
kuenenda kwa ROHO MTAKATIFU na kulisoma na kulitafarakri Neno la MUNGU.
Omba MUNGU akuvike vazi
la furaha
Zaburi 30:11 '' Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.''
Omba MUNGU kwamba majira
yako ya baraka yavikwe wema.
Zaburi 65:11 '' Umeuvika mwaka taji ya wema wako; Mapito yako yadondoza unono.''
Omba MUNGU awavike
fedheha wote waliokuonea kipepo.
Zaburi 109:29 '' Washitaki wangu watavikwa fedheha, Watajivika aibu yao kama joho.''.
Nakuomba pia unaposoma
somo hili andika points za kuombea, andika hata kama utapata points 20 za
kuombea andika hizo pembeni ili ukianza kuomba ugusie kila eneo la maisha yako.
Endelea kuishi maisha
matakatifu ya Wokovu wa Bwana YESU ili siku
ya mwisho uvikwe mwili mpya usioharibika wala kuzeeka.
1 Kor 15:53-54 '' Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.
Basi huu uharibikao
utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo
ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.
''
Omba MUNGU vazi la haki
alilokuvika lilete baraka kwako.
Maombi ya leo.
1.
Vua
mavazi yote ya kipepo uliyovalishwa na mawakala wa shetani kwenye ulimwengu wa
roho. Yataje mavazi hayo kupitia vifungo unavyoona umefungwa mfano magonjwa,
kuteswa n.k
2.
Choma
moto kwa damu ya YESU KRISTO kila vazi la kipepo ulilovalishwa na mawakala wa
shetani.
3.
Omba
MUNGU awavike fedheha maadui zako.
4.
Omba
MUNGU ili majira yako ya baraka yavikwe wema
5.
Omba
MUNGU kwamba vazi la haki alilokuvika likupe baraka
6.
Omba
MUNGU akuvike vazi la furaha.
7.
Funika
kwa damu ya YESU kila kitu chako ambacho kilikuwa kimevamiwa zamani na nguvu za
giza.
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane na nitakujulisha jinsi ya kukipata na Naamini kitakusaidia sana.
Hapa chini ni MAOMBI YA KULIVUA VAZI LA KIPEPO ULILOVIKWA NA MAWAKALA WA SHETANI.
Maombi haya naomba yamsaidie mtu yule ambaye hajui kuomba ili katika kuomba kwa kutumia hayo basi atakumbuka mahitaji yake na kuyataja katika maombi yake. Haya hapa chini ni maombi ya kuanzia tu katika maombi yako ili uendelee zaidi kuomba
Kwa waombaji wazoefu naamini baada tu ya kulisoma somo na kulielewa basi anajua aombee nini maana alikuwa anaandika points za kuombea. Kumbuka pia fundisho ni muhimu kuliko maombi hivyo wewe ambaye huwa unahusika na maombi tu hakikisha unajifunza kwanza somo lote ndipo utapata nguvu za kuomba na kushinda.
MAOMBI YA KULIVUA VAZI LA KIPEPO ULILOVIKWA NA MAWAKALA WA SHETANI.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane na nitakujulisha jinsi ya kukipata na Naamini kitakusaidia sana.
Hapa chini ni MAOMBI YA KULIVUA VAZI LA KIPEPO ULILOVIKWA NA MAWAKALA WA SHETANI.
Maombi haya naomba yamsaidie mtu yule ambaye hajui kuomba ili katika kuomba kwa kutumia hayo basi atakumbuka mahitaji yake na kuyataja katika maombi yake. Haya hapa chini ni maombi ya kuanzia tu katika maombi yako ili uendelee zaidi kuomba
Kwa waombaji wazoefu naamini baada tu ya kulisoma somo na kulielewa basi anajua aombee nini maana alikuwa anaandika points za kuombea. Kumbuka pia fundisho ni muhimu kuliko maombi hivyo wewe ambaye huwa unahusika na maombi tu hakikisha unajifunza kwanza somo lote ndipo utapata nguvu za kuomba na kushinda.
MAOMBI YA KULIVUA VAZI LA KIPEPO ULILOVIKWA NA MAWAKALA WA SHETANI.
Niko Mbele zako Eee YAHWEH MUNGU Muumbaji wangu, ninakushukuru sana kwa uzima ulionipa na ninakushukuru sana kwa nafasi hii njema ya kuomba mbele zako katika jina la YESU KRISTO Mwokozi aliye hai.
Niko pahali hapa BWANA naomba unisamehe dhambi zangu zote na uovu wangu wote na makosa yangu yote. Ninatubu kwako MUNGU Baba na naomba unisamehe Ee BWANA.
Namkataa shetani na kazi zake zote na kuanzia sasa mimi nitamtii Bwana YESU Mwokozi aliye hai.
Eee MUNGU Baba naamini nimepokea Msamaha wako maana ulisema tutubu kwa maana ufalme wako umekaribia kama Neno lako linavyosema katika Mathayo 3:2.
Nisaidie MUNGU wangu ili niishinde dhambi, nishinde machukizo ya dunia na nishinde kila hila ya shetani katika maisha yangu.
Niko sasa muda huu mahali hapa nikiyavua mavazi ya kipepo yote niliyovalishwa na maajenti wa kuzimu wote.
Kila vazi la kipepo nilivalishwa ili linitese katika ndoa, katika afya, katika uchumi na katika uzao, hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kukataliwa na kuonewa , hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kupata hasara kila mara katika biashara yangu hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kufuatiliwa na majini katika maisha yangu hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la balaa na majanga hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kuteswa na magonjwa hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la vifungo vya giza vyote hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kuondoa amani na furaha katika ndoa hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kukataliwa na wachumba hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kunizuia kupata kazi nzuri hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kuzuia uzao hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Tena sasa ninachoma kwa moto wa jina la YESU KRISTO kila vazi la kipepo lolote nililokuwa nimevalishwa, vazi hilo nalichoma kwa moto wa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kiroho la kipepo ambalo nimelivua leo kwa maombi sasa vazi hilo kwenye ulimwengu wa roho ninalichoma moto kwa damu ya YESU KRISTO aliye hai, na halitanirudia kamwe.
Naweka mpaka kwa damu ya YESU KRISTO kati yangu na ulimwengub wa roho wa giza, ninavunja kila muunganiko uliokuwepo kati yangu na ulimwengu wa roho wa giza, ninavunja kila muunganiko uliokuwepo kati ya baraka zangu, uchumi wangu, ardhi yangu na kila fursa yangu, huo muunganiko uliokuwepo kati ya vitu vyangu hivyo na ulimwengu wa roho wa giza ninauvunja kwa damu ya YESU KRISTO na katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Eee MUNGU Baba nakuomba uwavike fedheha maadui zangu wote katika ulimwengu wa roho, kama Neno lako BWANA linavyosema katika Zaburi 71:24 Kwamba '' Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.''
Kila wakala wa shetani ambaye aliwahi kunivika vazi la kipepo leo nimelivua vazi hilo, kwa jina la YESU KRISTO na nakuomba MUNGU Baba kwamba sasa uwapige kwa aibu na watahayarike sana maadui zangu wote katika ulimwengu wa roho.
Ninaomba wafedheheke na kuangamia wote waliokuwa wamenifunga katika afya yangu, uchumi wangu, ndoa yangu, uzao wangu na kibali changu.
Sasa Eee MUNGU Mwenyezi ninakuomba univike vazi la amani, furaha na baraka. Nivike Bwana YESU vazi lako la Wokovu na niishi maisha matakatifu siku zote katika wewe.
Kila baraka yangu popote iliko sasa naifunika kwa damu ya YESU KRISTO na mawakala wa kuzimu hawataigusa kamwe hiyo baraka yangu.
Niseme nini Bwana YESU? Bali ninashukuru tu maana ni leo umenipa Ushindi kupitia jina lako na damu yako ya agano na ya thamani kupita vyote.
Ninakushukuru JEHOVAH MUNGU wangu maana hakuna aliye kama wewe MUNGU wa Israeli.
Ni katika jina la YESU KRISTO nimeomba na ninashukuru.
Kila vazi la kuteswa na magonjwa hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la vifungo vya giza vyote hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kuondoa amani na furaha katika ndoa hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kukataliwa na wachumba hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kunizuia kupata kazi nzuri hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kuzuia uzao hilo vazi la kipepo ninalivua sasa kwa damu ya YESU KRISTO na kwa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Tena sasa ninachoma kwa moto wa jina la YESU KRISTO kila vazi la kipepo lolote nililokuwa nimevalishwa, vazi hilo nalichoma kwa moto wa jina la YESU KRISTO aliye hai.
Kila vazi la kiroho la kipepo ambalo nimelivua leo kwa maombi sasa vazi hilo kwenye ulimwengu wa roho ninalichoma moto kwa damu ya YESU KRISTO aliye hai, na halitanirudia kamwe.
Naweka mpaka kwa damu ya YESU KRISTO kati yangu na ulimwengub wa roho wa giza, ninavunja kila muunganiko uliokuwepo kati yangu na ulimwengu wa roho wa giza, ninavunja kila muunganiko uliokuwepo kati ya baraka zangu, uchumi wangu, ardhi yangu na kila fursa yangu, huo muunganiko uliokuwepo kati ya vitu vyangu hivyo na ulimwengu wa roho wa giza ninauvunja kwa damu ya YESU KRISTO na katika jina la YESU KRISTO aliye hai.
Eee MUNGU Baba nakuomba uwavike fedheha maadui zangu wote katika ulimwengu wa roho, kama Neno lako BWANA linavyosema katika Zaburi 71:24 Kwamba '' Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.''
Kila wakala wa shetani ambaye aliwahi kunivika vazi la kipepo leo nimelivua vazi hilo, kwa jina la YESU KRISTO na nakuomba MUNGU Baba kwamba sasa uwapige kwa aibu na watahayarike sana maadui zangu wote katika ulimwengu wa roho.
Ninaomba wafedheheke na kuangamia wote waliokuwa wamenifunga katika afya yangu, uchumi wangu, ndoa yangu, uzao wangu na kibali changu.
Sasa Eee MUNGU Mwenyezi ninakuomba univike vazi la amani, furaha na baraka. Nivike Bwana YESU vazi lako la Wokovu na niishi maisha matakatifu siku zote katika wewe.
Kila baraka yangu popote iliko sasa naifunika kwa damu ya YESU KRISTO na mawakala wa kuzimu hawataigusa kamwe hiyo baraka yangu.
Niseme nini Bwana YESU? Bali ninashukuru tu maana ni leo umenipa Ushindi kupitia jina lako na damu yako ya agano na ya thamani kupita vyote.
Ninakushukuru JEHOVAH MUNGU wangu maana hakuna aliye kama wewe MUNGU wa Israeli.
Ni katika jina la YESU KRISTO nimeomba na ninashukuru.
Amen Amen Ameeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeen.
Hakika umeshinda. Ukiweza kufunga unaweza kufunga hata siku 1 au 3 au 3 au hata 5 au zile ambazo wewe utaona unaweza ukihusika kila siku na kipengele kimoja kuombea na kumbuka baada ya maombi ya kufunga au hata maombi ya bila kufunga fanya tendo la imani kwa MUNGU kwa kutoa sadaka nzuri itakayoambatana na maombi juu ya ukomo wa kuteswa na maadui zako katika ulimwengu wa roho
Nawaonya pia wanaotumia masomo yangu vibaya na kwa manufaa yao waache tabia hiyo.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Hakika umeshinda. Ukiweza kufunga unaweza kufunga hata siku 1 au 3 au 3 au hata 5 au zile ambazo wewe utaona unaweza ukihusika kila siku na kipengele kimoja kuombea na kumbuka baada ya maombi ya kufunga au hata maombi ya bila kufunga fanya tendo la imani kwa MUNGU kwa kutoa sadaka nzuri itakayoambatana na maombi juu ya ukomo wa kuteswa na maadui zako katika ulimwengu wa roho
Nawaonya pia wanaotumia masomo yangu vibaya na kwa manufaa yao waache tabia hiyo.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa BWANA YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la BWANA YESU.
0714252292.
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Comments