Na Peter M Mabula. Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU. |
JINSI YA KUTOKA KWENYE VIFUNGO VYA GIZA
Bwana YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze Neno la MUNGU.
Leo
tunajifunza jinsi ya kutoka katika vifungo vya kishetani.
Kifungo cha
kipepo ni nini?
Kifungo cha
kipepo ni adhabu ya mtu kuwekwa jela kipepo na mawakala wa shetani.
Jela ni
mahali wanapowekwa waharifu ili watumikie adhabu.
Wako watu
wengi tu wanateswa na vifungo vya giza katika maisha yao, wengine wanatamani
watoke katika vifungo hivyo lakini imeshindikana maana hawaijui njia sahihi ya kuwatoa katika vifungo..
Jambo la
kwanza kabisa nataka kukuambia ni kwamba Bwana YESU alikuja ili kuzivunja na
kuziharibu kazi zote za shetani vikiwemo vifungo vya kipepo.
1 Yohana
3:8b ''Kwa kusudi hili Mwana wa MUNGU alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. ''
Kuna mambo
mengi yanaweza yakahitajika ili hadi mtu husika afunguliwe kutoka vifungo vya
giza.
Kufunguliwa
vifungo kunahitaji maombi sahihi, kujitambua, kujielewa, kutii Neno la MUNGU na kuenenda katika ROHO MTAKATIFU.
Kuna vifungo
vingi vya giza ambavyo watu wengi wamefungwa kichawi.
Baadhi ya
vifungo hivyo vimetajwa katika Isaya
42:22 ''Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika
mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana
aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha.
'' acha nikifafanulie.
Vifungo
hivyo vya giza ni hivi.
1. Kuibiwa
ufahamu kipepo ili ulitumikie kusudi la shetani na sio la MUNGU.
''Lakini watu hawa ni watu walioibiwa ''
Kuna watu wengi fahamu zao zimefunga kipepo kiasi kwamba wanalitumikia kusudi la shetani na sio la MUNGU, Leo kwa njia ya maombi yako katika jina la YESU KRISTO hakikisha unakiharibu kifungo hicho cha giza kilichokufunga ufahamu.
Kuna watu wengi fahamu zao zimefunga kipepo kiasi kwamba wanalitumikia kusudi la shetani na sio la MUNGU, Leo kwa njia ya maombi yako katika jina la YESU KRISTO hakikisha unakiharibu kifungo hicho cha giza kilichokufunga ufahamu.
Fikra zako zinatakiwa zimtii KRISTO na sio kutii majini na
mizimu.
2 Kor 10:3-5 '' Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika MUNGU hata kuangusha ngome;)
tukiangusha mawazo na kila kitu
kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya MUNGU; na tukiteka nyara kila
fikira ipate kumtii KRISTO;
''
2. Kutekwa
na nguvu za giza.
''Lakini watu hawa ni watu waliotekwa''
''Lakini watu hawa ni watu waliotekwa''
Baadhi ya dalili ya mtu aliye katika kifungo cha kutekwa na nguvu za giza
ni kuonewa sana na majini au wachawi kwa sababu tu wamekuteka katika ulimwengu
wa roho.
Somo linaitwa jinsi ya kutoka kwenye vifungo vya giza, ni muhimu kujua
kwamba kila kifungo kina kanuni zake hadi utoke katika kifungo hicho, kuna
vifungo vingine huhitaji hata maombi bali unahitaji tu kubadilika tabia na
kifungo hicho kinaondoka.
3.Kunaswa
katika mashimo ya giza.
''Lakini watu hawa ni watu walionaswa katika
mashimo''
Inawezekana wewe uko katika kifungo cha mashimo ya giza.
Inawezekana wewe uko katika kifungo cha mashimo ya giza.
Inawezekana uko katika shimo la dhambi.
Inawezekana wewe uko katika shimo la madeni au kufilisika.
Inawezekana wewe uko katika shimo la madeni au kufilisika.
Inawezekana umenaswa katika shimo la magonjwa na hadi kwa sasa unadhani
hutapona kabisa kulingana na jinsi unavyouona ugonjwa wako.
Inawezekana uko katika shimo la kifo ili siku chache zijazo upate ajali
mbaya waliyoipanga wachawi na wakuu wa giza ili ikupate.
Wakati mwingine kupitia ndoto ambazo unaota unakuwa unajulishwa aina ya
kifungo ambacho umefungwa ili ujue jinsi ya kutoka katika kifungo hicho.
Inawezekana wewe huota ndoto kabisa ukiwa ndani ya shimo refu sana na
huoni pa kutokea, hapo unaonyeshwa aina ya kifungo kinachokutesa.
Ndugu, leo katika jina la YESU KRISTO nakuomba kimbilia maombezi
makanisani na utaombewa na kifungo hicho kukuacha.
4. Kufichwa
katika magereza.
''Lakini watu hawa ni watu waliofichwa katika magereza ''
Kuna kifungo cha giza kinaitwa gereza.
Kuna kifungo cha giza kinaitwa gereza.
Inawezekana wewe uko katika gereza la magaonjwa, kukataliwa,kudhalauliwa
bila sababu, kutengwa n.k
Inawezekana ndoa yako iko gerezani, inawezekana uchumba wako uko gerezani,
iinawezekana biashara yako au wito wako viko gerezani
Ndugu leo hakikisha unandoka katika gereza la kipepo ulimofungwa kipepo.
5. Kuwa Mawindo ya nguvu za giza.
''Lakini watu hawa ni watu ambaob wamekuwa mawindo, ''
Kuna kifungo kinaitwa mawindo, inawezekana wewe siku zote uko katika mawindo ya majini au wachawi.
Kuna kifungo kinaitwa mawindo, inawezekana wewe siku zote uko katika mawindo ya majini au wachawi.
Kuna watu huwa hawalali usiku kwa sababu wako katika mawindo ya wachawi
na majini.
Mama mmoja kutoka nchi jirani siku moja alinipigia simu ili nimuombee,
nilipomuombea kesho yake alituma sadaka kisha akasema hivi ‘’ Mtumishi Mabula huwezi
kuamini mimi na mtoto wangu tuna zaidi ya miezi miwili bila kulala usiku, jana
uliponiombea ndio nilishangaa maana nilipojaribu kulala nikashtuka nikidhani
wachawi sasa wanakuja kumbe ili asubuhi saa mbili yaani nililala salama kwa
mara ya kwanza’’
Mama Yule aliniambia kwamba alikosana na Baba mmoja mfuga majini ambaye
alimwambia kwamba hatalala usiku hata siku moja, kifungo kile kilimtesa sana
lakini baada ya maombi kifungo kiliondoka.
Ndugu uko katika mawindo gani?
Kuna watu kila siku ni kukabwa tu na majinamizi.
Kuna mtu kila ugonjwa ukitokea na yeye lazima aumwe.
Kuna watu huchapwa viboko usingizini.
Ndugu, uko kwenye mawindo gani ya kipepo?
Leo katika jina la YESU KRISTO kataa kuwa mawindo.
Kwa maombi yako, wachawi au majini wanaweza kukuogopa na wasikufuatilie
tena maisha yako yote, kama ukiomba inavyotakiwa.
Maombi ya vita ni ya muhimu sana ili utoke katika vifungo vya giza, watu
wengi hawaelewi jambo hilo wakidhani kwamba shetani unaweza ukambeleleza
kutoka, ndugu yangu, mashetani huwa hayabembelezwi kutoka bali toa amri kwa
jina la YESU kwamba watoke na watatoka hakika, usiombe kistaarabu sana kila
maombi yako.
Nguvu za giza zinaondolewa kwa nguvu na sio vinginevyo.
Mathayo 18:18 '' Amin, nawaambieni, yo yote
mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote
mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.
''
Ndugu kumbuka kwamba YESU alikuwa anaziamuru nguvu za giza ziwatoke watu
na zinatoka.
Mitume walikuwa wanaziamuru nguvu za giza ziwatoke watu na zinawatoka, mbona wewe unazibembeleza nguvu za giza kutoka?
Kama kuna jambo muhimu sana ukitaka kutoka katika vifungo vya giza ni
muhimu sana ukaenda kuombewa
ROHO MTAKATIFU ni muhimu sana ili ajulishe jinsi ya kutoka katika vifungo
vya giza, ndio maana unapaswa pia kuwashirikisha watumishi wa MUNGU.
Mwanamke mmoja aliota ndoto
amefungwa kipepo ili asizae, lakini hakuwa amefungwa kifungo kimoja tu
bali alikuwa amefungwa vifungo saba vyote kwa ajili ya kumzuia kuzaa. Ndugu,
Bila ROHO MTAKATIFU unaweza kuwa unapambana na kifungo kimoja kila mwaka hivyo
baada ya miaka 7 ndipo vitaisha hivyo vifungo, na kama ulianza kuomba ndoa yako
ikiwa na miaka 2 maana yake unaweza kupata uzao ndoa ikiwa na miaka 9.
Je kama ndoa yako ulianza kuomba ikiwa na miaka 7, utakuja kuzaa ndoa
ikiwa na umri gani?
Ndugu, leo fungua kila kifungo kwa damu ya YESU KRISTO ya agano.
Nyunyuzia damu ya YESU ili ikapeleleze katika ardhi ulikofungwa au katika
bahari ulikofungwa au popote ili hicho
kifungo kiondoke.
Kuna binti yeye alivalishwa pete za kichawi kila kidole cha mkono wake,
aliona kwenye ndoto lakini hakujali.
Pete zile ni maagano ya kishetani kati yake na majini mahaba ili
kumzuilia kuolewa.
Ndugu kwa YESU ni sehemu pekee salama ambapo unaweza kufunguliwa vifungo
vya giza vyote.
Ukimwamini na maombi katika jina lake hakika utafunguliwa.
Ukimwamini na maombi katika jina lake hakika utafunguliwa.
Marko 9:23 ''YESU akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.''
Jambo la kujua ni kwamba kila kifungo kina njia zake za kutoka katika
kifungo hicho, kama unajua kifungo ulichofungwa basi tafuta kujua jinsi ya
kutoka katika kifungo hicho.
Kuna vifungo unahitaji tu kubadilika tabia baada ya kutubu ndipo
vinaondoka.
Kuna vifungo unahitaji kujulishwa na Neno la MUNGU jinsi ya kutoka.
Kuna vifungo vinahitaji sadaka na maombi ili kutoka katika vifungo hivyo.
Ngoja nikupe namna ya kutoka katika baadhi ya vifungo vya kipepo maana
kila kifungo kina kanuni zake za kutoka katika vifungo hivyo.
Hivi ni baadhi tu lakini wewe ndio unajua kifungo kinachokutesa hivyo tafuta kujua jinsi ya kutoka katika kifungo hicho na hakika katika jina la YESU KRISTO utatoka katika kifungo hicho.
Hivi ni baadhi tu lakini wewe ndio unajua kifungo kinachokutesa hivyo tafuta kujua jinsi ya kutoka katika kifungo hicho na hakika katika jina la YESU KRISTO utatoka katika kifungo hicho.
A.
Jinsi ya kutoka kwenye kifungo cha magonjwa.
1.
Tubu
kwa kilichosababisha ufungwe kifungo cha magonjwa.
Matendo 3:19 '' Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA; ''
Matendo 3:19 '' Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake BWANA; ''
2.
Amuru
ugonjwa utoke ndani yako.
Mathayo 18:18 '' Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. ''
Mathayo 18:18 '' Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. ''
3.
Omba
MUNGU akuponye.
Mathayo 7:8 '' kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. ''
Mathayo 7:8 '' kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. ''
4.
Isemeshe
nafsi yako kwamba unapona.
Zaburi 116:7 '' Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako, Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.''
Zaburi 116:7 '' Ee nafsi yangu, urudi rahani mwako, Kwa kuwa BWANA amekutendea ukarimu.''
5.
Ita
afya itokayo kwa MUNGU.
Yeremia 33:6 ''Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.''
Yeremia 33:6 ''Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.''
B.
Jinsi ya kutoka katika vifungo vya dhambi.
1.
Tubu
na kuziacha dhambi zote.
Zaburi 34:14 ''Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.''
Zaburi 34:14 ''Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.''
2.
Vunja uhusiano
na watu ulioshirikiana nao kwenye
dhambi.
Zaburi 1:1 '' Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.''
Zaburi 1:1 '' Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.''
3.
Amua
kuwa mtu wa ibada na maombi.
Yohana 4:24 ''MUNGU ni ROHO, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. ''
Yohana 4:24 ''MUNGU ni ROHO, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli. ''
4.
Ishi
maisha matakatifu ya wokovu wa KRISTO YESU.
1 Petro 1:15 '' bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; ''
1 Petro 1:15 '' bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; ''
5.
Usikumbuke
mambo ya kwanza yaani mambo ya dhambi.
Isaya 43:18 ''Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.''
Isaya 43:18 ''Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.''
6.
Enenda
kwa ROHO MTAKATIFU.
Warumi 8:14 ''Kwa kuwa wote wanaoongozwa na ROHO wa MUNGU, hao ndio wana wa MUNGU.''
Warumi 8:14 ''Kwa kuwa wote wanaoongozwa na ROHO wa MUNGU, hao ndio wana wa MUNGU.''
7.
Haribu
kwa damu ya YESU kila madhabahu ya giza au nguvu za giza zilizokuwa
zinakutumikisha kufanya dhambi.
Kumb 7:5 '' Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.''
Kumb 7:5 '' Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.''
C.
Vifungo
vya madeni.
1.
Omba
MUNGU upate pesa ya kulipa kisha lipa deni hilo.
2.
Epuka
kukopa
3.
Omba
MUNGU akubariki na fanya kazi kwa bidii
ili uwe na pesa zako mwenyewe.
4.
Haribu
kila nguvu za giza zinazoleta uharibifu maishani mwako ili ukope pesa
kushughulikia matatizo yako.
D.Vifungo vya ajali au balaa au mikosi.
1.
Haribu
kwa maombi kila watenda kazi ya kishetani wanaotumika kuleta ajali, mikosi au
balaa kwako.
2.
Haribu
madhabahu za giza zinazoleta mambo yao
kwako.
3.
Mtegemee
MUNGU na kumtumaini kisha omba yeye
akulinde. Isaya 26:3 ''Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea Katika amani kamilifu, kwa kuwa anakutumaini.
''.
Kila siku omba katika jina la YESU na kabla ya jambo lolote au safari yeyote omba kwa MUNGU.
Kila siku omba katika jina la YESU na kabla ya jambo lolote au safari yeyote omba kwa MUNGU.
4.
Msikilize
ROHO MTAKATIFU ili kama kuna mahali hatakupa amani kwenda basi uusiende.
E.
Kifungo
cha utasa.
1.
Omba
Bwana YESU akufungue kifungo hicho huku ukitumia damu ya YESU maana hujui ni
wapi ulifungwa.
Yohana 14:14 ''Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. ''
Yohana 14:14 ''Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya. ''
2.
Haribu
kila nguvu za giza zilizoitumika kukuzuilia uzao.
Luka 10:19 '' Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. ''
Luka 10:19 '' Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. ''
3.
Futa
kila maneno ya watu mabaya waliyokutamkia ili kukuzuia uzao.
Yakobo 3:5 ''Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. ''
Yakobo 3:5 ''Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. ''
4.
Fungua
tumbo lako la uzazi kwa maombi na takasa kila sehemu ya mwili wako na ya
mume/mke wako inayohusika na uzao.
Waamuzi 13:3 '' Malaika wa BWANA akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, WEWE SASA U TASA, HUZAI; LAKINI UTACHUKUA MIMBA, NAWE UTAPATA MTOTO mwanamume. ''
Waamuzi 13:3 '' Malaika wa BWANA akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, WEWE SASA U TASA, HUZAI; LAKINI UTACHUKUA MIMBA, NAWE UTAPATA MTOTO mwanamume. ''
5.
Ita
uzao wako kwa jina la YESU KRISTO.
Mathayo 12:37 '' KWA KUWA KWA MANENO YAKO UTAHESABIWA HAKI, na kwa maneno yako utahukumiwa.''
Mathayo 12:37 '' KWA KUWA KWA MANENO YAKO UTAHESABIWA HAKI, na kwa maneno yako utahukumiwa.''
6.
Ukomboe
uzao wako uliozuiliwa kipepo ili usije.
Zaburi 91:10 '' Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako. ''
Zaburi 91:10 '' Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako. ''
7.
Mpinge
shetani na kazi zake zote na uwe mtu wa maombi.
Zaburi 91:13 '' Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.''
Zaburi 91:13 '' Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.''
8.
Omba
kwa MUNGU kwamba majira yako ya kupata uzao yaje na asizuie yeyote.
Mhubiri 3:1 '' Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.''
Mhubiri 3:1 '' Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.''
9.
Ishi
maisha ya uaminifu katika ndoa yako huku ukifanyia kazi kimaombi kila unachoona
kwenye ndoto au maono kinachohusika na uzao.
Waebrania 13:4 '' Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu. ''
Waebrania 13:4 '' Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi MUNGU atawahukumia adhabu. ''
10. Ita
ahadi ya MUNGU ya uzao kwako ili itimie.
Mwanzo 18:14 ''Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. ''
Mwanzo 18:14 ''Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume. ''
11.
Omba
nguvu za MUNGU zikufunike siku zote.
Isaya 40:29-31 ''Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.''
Isaya 40:29-31 ''Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.''
12. Omba
kujua mapenzi/Matakwa ya MUNGU juu ya
uzao wako.
Isaya 14:27 ''Maana BWANA wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?''
Somo lina ufafanuzi mwingi sana hivyo siku moja nitalifafanua zaidi katika kitabu ambacho nitachapisha na kitakufikia.
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Isaya 14:27 ''Maana BWANA wa majeshi amekusudia, naye ni nani atakayelibatili? Na mkono wake ulionyoshwa, ni nani atakayeugeuza nyuma?''
Somo lina ufafanuzi mwingi sana hivyo siku moja nitalifafanua zaidi katika kitabu ambacho nitachapisha na kitakufikia.
Natamani niseme mengi mno lakini naamini mwenye kuelewa ameelewa.
MUNGU akubariki kwa kujifunza somo hili muhimu pia kitabu changu cha MAOMBI YA KINA kinapatikana, tuwasiliane nitakujulisha jinsi ya kukipata.
Asante kama umelielewa Neno la MUNGU la siku ya leo ila nina neno moja la mwisho kwako leo.
BWANA YESU Amekaribia Kurudi.
Je, Umejiandaaje?
Je, Unaendeleza Dhambi Ili Siku Ile Uachwe Na BWANA YESU? Je, Umeshika Wokovu Na Utakatifu Hata Unyakuliwe Siku Ile Kwa Ajili Ya Kwenda Uzima Wa Milele?
Majibu Sahihi Yako Moyoni Mwako Ila Nakusihi Mpokee BWANA YESU Kama Hujampokea Na Nakusihi Ishi Maisha Matakatifu Ukiwa Ndani Ya Wokovu.
Vya Dunia Tulivikuta Na Tutaviacha.
Ndugu, Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Kuokoka.
Vya Dunia Visikupotezee Muda Wako Hata Ukasahau Wokovu Wa Bwana YESU Kwako.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
Mtenda kazi katika shamba la Bwana YESU.
0714252292(Hadi whatsapp).
0786719090
mabula1986@gmail.com
Nakuomba share kwa marafiki zako ujumbe huu.
Comments