![]() | |
|
| Bwana YESU KRISTO Mwokozi atukuzwe. |
Karibu tujifunze ujumbe huu mfupi.
Unamkumbuka yule Punda aliyembeba Bwana YESU KRISTO?.
◼️Punda yule alipita hadi sehemu asiyotakiwa kwa sababu tu alikuwa amembeba Bwana YESU.
◼️Punda alipita kwenye barabara ambayo imetandikwa nguo nzuri za thamani kwa sababu tu punda alikuwa amembeba Bwana YESU KRISTO.
Mathayo 21:6-9 " Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama YESU alivyowaamuru, wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake. Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani. Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la BWANA; Hosana juu mbinguni.
◼️Punda alipata heshima ya kupita juu ya nguo nzuri kwa sababu tu alikuwa amembeba Bwana YESU KRISTO Mwokozi.
➡️Nini nataka kusema?
◼️Wewe ukimbeba Bwana YESU moyoni Mwako unaweza ukapita hata kwenye ngome za wachawi lakini hawatakufanya lolote kwa sababu umembeba YESU KRISTO asiyeshindwa.
◼️Ndugu kama ukimbeba YESU KRISTO moyoni mwako unaweza kuishi hata sehemu ambazo wengine wanasema Mwanadamu Fulani hawezi kuishi eneo hilo kwa sababu eneo hilo ni makao ya nguvu za giza.
◼️Ndugu, mbebe Bwana YESU KRISTO katika Maisha Yako utapita kila sehemu na nguvu za giza hazitakugusa.
➡️Unambebaje Bwana YESU?
◼️Unambeba Bwana YESU KRISTO Kwa kumpokea kama Mwokozi wako Kisha ukafuata maelekezo yake.
Yohana 1:12-13 " Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU."
Tena ukimpokea Bwana YESU KRISTO yeye na Baba yake watakuja kwako na kufanya makazi hivyo utapata heshima kama aliyoipata yule Punda na zaidi.
Yohana 14:23 "YESU akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na BABA yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake."
Ndugu, ni wakati wako wa kupata heshima na kuogopekwa kwa mawakala wa shetani kwa sababu una Bwana YESU KRISTO kama Mwokozi wako.
Nakuomba Mpokee Bwana YESU KRISTO kama Mwokozi wako na ataanza kuwa kwako hivyo utashinda na zaidi na kushinda na utapata heshima maana uko na yeye Mwokozi mwenye Nguvu na heshima.
MUNGU wa Mbinguni akubariki sana.
By Mwl Peter Mabula
Mtenda kazi katika Shamba la MUNGU Mwenyezi.
Amen.

Comments